Zaburi 36:1-12
Kwa kiongozi. Ya mtumishi wa Yehova, Daudi.
36 Maneno ya ukosaji kwa mtu mwovu yako katikati ya moyo wake;+Hakuna hofu ya Mungu mbele ya macho yake.+
2 Kwa maana ametenda kwa ulaini machoni pake mwenyewe+Asiweze kuliona kosa lake ili alichukie.+
3 Maneno ya kinywa chake ni kuumiza na udanganyifu;+Ameacha kuwa na ufahamu wa kufanya mema.+
4 Yeye anaendelea kupanga hila ya kuumiza kitandani mwake.+Husimama katika njia isiyo nzuri.+Hakatai lililo baya.+
5 Ee Yehova, fadhili zako zenye upendo ziko mbinguni;+Uaminifu wako umefika mawinguni.+
6 Uadilifu wako ni kama milima ya Mungu;+Uamuzi wako wa hukumu ni kilindi kikubwa cha maji.+Wewe huokoa mwanadamu na mnyama, Ee Yehova.+
7 Jinsi zilivyo na thamani fadhili zako zenye upendo, Ee Mungu!+Nao wana wa binadamu hupata kimbilio katika kivuli cha mabawa yako.+
8 Wao hunywa na kushiba vinono vya nyumba yako;+Nawe huwanywesha kwenye mito ya raha zako.+
9 Kwa maana kwako wewe iko chemchemi ya uzima;+Kwa nuru inayotoka kwako sisi tunaweza kuona nuru.+
10 Endeleza fadhili zako zenye upendo kwa wale wanaokujua,+Na uadilifu wako kwa wale walio wanyoofu moyoni.+
11 Mguu wa majivuno usinijie;+Nao mkono wa watu waovu, usinifanye kuwa mtu wa kutanga-tanga.+
12 Huko wanaotenda mambo yenye kuumiza wameanguka;+Wamesukumwa chini nao wameshindwa kusimama.+