Zaburi 83:1-18

Wimbo. Muziki wa Asafu.+ 83  Ee Mungu, usinyamaze;+Usikae bila kusema, wala kukaa kimya, Ee Mungu.+   Kwa maana, tazama! adui zako wanafanya fujo;+Na wale wanaokuchukia vikali wameinua kichwa chao.+   Wanaendeleza kwa ujanja mazungumzo ya siri juu ya watu wako;+Nao wanapanga hila juu ya watu wako waliofichwa.+   Wamesema: “Njooni, tuwafutilie mbali wasiwe taifa,+Ili jina la Israeli lisikumbukwe tena.”+   Kwa maana kwa moyo wameshauriana kwa umoja;+Naam, wakafanya agano dhidi yako,+   Mahema ya Edomu+ na Waishmaeli, Moabu+ na Wahagri,+   Gebali na Amoni+ na Amaleki,Ufilisti+ pamoja na wakaaji wa Tiro.+   Pia, Ashuru imejiunga nao;+Wamekuwa mkono kwa wana wa Loti.+ Sela.   Uwatendee kama Midiani,+ kama Sisera,+Kama Yabini+ kwenye bonde la mto la Kishoni.+ 10  Waliangamizwa huko En-dori;+Wakawa mbolea kwa ajili ya udongo.+ 11  Na uwafanye watu wao wenye vyeo wawe kama Orebu na kama Zeebu,+Na watawala wao wadogo wote kama Zeba na kama Zalmuna,+ 12  Ambao wamesema: “Na tumiliki makao ya Mungu.”+ 13  Ee Mungu wangu, uwafanye kama kisulisuli cha mbaruti,+Kama majani makavu mbele ya upepo.+ 14  Kama moto unaoteketeza msitu+Na kama mwali wa moto unaounguza milima,+ 15  Uwafuatilie vivyo hivyo tu kwa tufani yako+Nawe uwasumbue kwa upepo wako wenye dhoruba.+ 16  Ujaze nyuso zao aibu,+Ili watu wapate kulitafuta jina lako, Ee Yehova.+ 17  Na waone aibu na kusumbuka nyakati zote,+Nao wafedheheshwe na kuangamia;+ 18  Ili watu wajue+ kwamba wewe, ambaye jina lako ni Yehova,+Wewe peke yako ndiye Uliye Juu Zaidi,+ juu ya dunia yote.+

Maelezo ya Chini