Zaburi 83:1-18
Wimbo. Muziki wa Asafu.+
83 Ee Mungu, usinyamaze;+Usikae bila kusema, wala kukaa kimya, Ee Mungu.+
2 Kwa maana, tazama! adui zako wanafanya fujo;+Na wale wanaokuchukia vikali wameinua kichwa chao.+
3 Wanaendeleza kwa ujanja mazungumzo ya siri juu ya watu wako;+Nao wanapanga hila juu ya watu wako waliofichwa.+
4 Wamesema: “Njooni, tuwafutilie mbali wasiwe taifa,+Ili jina la Israeli lisikumbukwe tena.”+
5 Kwa maana kwa moyo wameshauriana kwa umoja;+Naam, wakafanya agano dhidi yako,+
6 Mahema ya Edomu+ na Waishmaeli, Moabu+ na Wahagri,+
7 Gebali na Amoni+ na Amaleki,Ufilisti+ pamoja na wakaaji wa Tiro.+
8 Pia, Ashuru imejiunga nao;+Wamekuwa mkono kwa wana wa Loti.+ Sela.
9 Uwatendee kama Midiani,+ kama Sisera,+Kama Yabini+ kwenye bonde la mto la Kishoni.+
10 Waliangamizwa huko En-dori;+Wakawa mbolea kwa ajili ya udongo.+
11 Na uwafanye watu wao wenye vyeo wawe kama Orebu na kama Zeebu,+Na watawala wao wadogo wote kama Zeba na kama Zalmuna,+
12 Ambao wamesema: “Na tumiliki makao ya Mungu.”+
13 Ee Mungu wangu, uwafanye kama kisulisuli cha mbaruti,+Kama majani makavu mbele ya upepo.+
14 Kama moto unaoteketeza msitu+Na kama mwali wa moto unaounguza milima,+
15 Uwafuatilie vivyo hivyo tu kwa tufani yako+Nawe uwasumbue kwa upepo wako wenye dhoruba.+
16 Ujaze nyuso zao aibu,+Ili watu wapate kulitafuta jina lako, Ee Yehova.+
17 Na waone aibu na kusumbuka nyakati zote,+Nao wafedheheshwe na kuangamia;+
18 Ili watu wajue+ kwamba wewe, ambaye jina lako ni Yehova,+Wewe peke yako ndiye Uliye Juu Zaidi,+ juu ya dunia yote.+