Zaburi 136:1-26
136 Mshukuruni Yehova, kwa maana ni mwema:+Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo;+
2 Mshukuruni Mungu wa miungu:+Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo;+
3 Mshukuruni Bwana wa mabwana:+Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo;+
4 Yule peke yake aliye Mtendaji wa mambo ya ajabu, mambo makuu:+Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo;+
5 Yule anayezifanya mbingu kwa uelewaji:+Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo;+
6 Yule anayeitandaza dunia juu ya maji:+Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo;+
7 Yule anayeifanya ile mianga mikubwa:+Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo;+
8 Naam, jua ili litawale wakati wa mchana:+Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo;+
9 Mwezi na nyota ili zitawale pamoja wakati wa usiku:+Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo;+
10 Yule anayepiga Misri katika wazaliwa wao wa kwanza:+Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo;+
11 Na Yule anayetoa Israeli kutoka katikati yao:+Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo;+
12 Kwa mkono wenye nguvu na kwa mkono ulionyooshwa:+Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo;
13 Yule anayekata Bahari Nyekundu sehemu-sehemu:+Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo;+
14 Na aliyefanya Israeli wapite katikati yake:+Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo;+
15 Na aliyemkung’uta Farao na jeshi lake ndani ya Bahari Nyekundu:+Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo;+
16 Yule anayetembeza watu wake kupita nyikani:+Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo;+
17 Yule anayepiga wafalme wakubwa:+Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo;+
18 Na ambaye aliua wafalme wenye fahari:+Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo;+
19 Naam, Sihoni mfalme wa Waamori:+Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo;+
20 Na Ogu mfalme wa Bashani:+Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo;+
21 Na ambaye aliitoa nchi yao iwe urithi:+Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo;+
22 Urithi kwa Israeli mtumishi wake:+Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo;+
23 Ambaye alitukumbuka tulipokuwa katika hali ya chini:+Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo;+
24 Na ambaye alitunyakua kutoka kwa adui zetu tena na tena:+Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo;+
25 Yule anayewapa chakula wote wenye mwili:+Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo;+
26 Mshukuruni Mungu wa mbinguni:+Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo.+