Zaburi 136:1-26

136  Mshukuruni Yehova, kwa maana ni mwema:+Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo;+   Mshukuruni Mungu wa miungu:+Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo;+   Mshukuruni Bwana wa mabwana:+Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo;+   Yule peke yake aliye Mtendaji wa mambo ya ajabu, mambo makuu:+Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo;+   Yule anayezifanya mbingu kwa uelewaji:+Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo;+   Yule anayeitandaza dunia juu ya maji:+Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo;+   Yule anayeifanya ile mianga mikubwa:+Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo;+   Naam, jua ili litawale wakati wa mchana:+Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo;+   Mwezi na nyota ili zitawale pamoja wakati wa usiku:+Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo;+ 10  Yule anayepiga Misri katika wazaliwa wao wa kwanza:+Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo;+ 11  Na Yule anayetoa Israeli kutoka katikati yao:+Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo;+ 12  Kwa mkono wenye nguvu na kwa mkono ulionyooshwa:+Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo; 13  Yule anayekata Bahari Nyekundu sehemu-sehemu:+Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo;+ 14  Na aliyefanya Israeli wapite katikati yake:+Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo;+ 15  Na aliyemkung’uta Farao na jeshi lake ndani ya Bahari Nyekundu:+Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo;+ 16  Yule anayetembeza watu wake kupita nyikani:+Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo;+ 17  Yule anayepiga wafalme wakubwa:+Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo;+ 18  Na ambaye aliua wafalme wenye fahari:+Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo;+ 19  Naam, Sihoni mfalme wa Waamori:+Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo;+ 20  Na Ogu mfalme wa Bashani:+Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo;+ 21  Na ambaye aliitoa nchi yao iwe urithi:+Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo;+ 22  Urithi kwa Israeli mtumishi wake:+Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo;+ 23  Ambaye alitukumbuka tulipokuwa katika hali ya chini:+Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo;+ 24  Na ambaye alitunyakua kutoka kwa adui zetu tena na tena:+Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo;+ 25  Yule anayewapa chakula wote wenye mwili:+Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo;+ 26  Mshukuruni Mungu wa mbinguni:+Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo.+

Maelezo ya Chini