Zaburi 71:1-24

71  Nimekukimbilia wewe, Ee Yehova.+Nisiaibike kamwe.+   Unikomboe kwa uadilifu wako na kuniokoa.+Tega sikio lako kwangu na uniokoe.+   Uwe kwangu ngome ya mwamba ya kuingia ndani daima.+Utoe amri ili kuniokoa,+Kwa maana wewe ni mwamba wangu na ngome yangu.+   Ee Mungu wangu, uniokoe na mkono wa mwovu,+Na mkono wa mtu anayetenda kwa njia isiyo ya haki na kwa ukandamizaji.+   Kwa maana wewe ni tumaini langu,+ Ee Bwana Mwenye Enzi Kuu, Yehova, tegemeo langu tangu ujana wangu.+   Nimekutegemea tangu tumboni;+Wewe ndiye Yule anayenitenganisha na sehemu za ndani za mama yangu.+Sifa yangu kwako ni ya daima.+   Nimekuwa kama muujiza kwa watu wengi;+Lakini wewe ni kimbilio langu lenye nguvu.+   Kinywa changu kimejawa na sifa zako,+Mchana kutwa na uzuri wako.+   Usinitupe wakati wa uzee;+Wakati tu nguvu zangu zinapungua, usiniache.+ 10  Kwa maana adui zangu wamesema juu yangu,+Na walewale wanaoitafuta nafsi yangu wameshauriana pamoja,+ 11  Wakisema: “Mungu mwenyewe amemwacha.+Mfuatilieni na kumkamata, kwa maana hakuna mkombozi.”+ 12  Ee Mungu, usikae mbali nami.+Ee Mungu wangu, ufanye haraka kunisaidia.+ 13  Hao na waaibike, hao na wafikie mwisho wao, wanaoshindana na nafsi yangu.+Hao na wajifunike kwa shutuma na fedheha wanaonitafutia msiba.+ 14  Lakini mimi, nitangoja daima,+Nami nitaongezea sifa zako zote. 15  Kinywa changu mwenyewe kitasimulia uadilifu wako,+Wokovu wako mchana kutwa,+Kwa maana sijapata kujua hesabu yake.+ 16  Nitaingia na nguvu kuu,+ Ee Bwana Mwenye Enzi Kuu+ Yehova;Nitautangaza uadilifu wako, naam, wako peke yako.+ 17  Ee Mungu, umenifundisha tangu ujana wangu,+Na mpaka sasa ninaendelea kutangaza kazi zako za ajabu.+ 18  Na mpaka wakati wa uzee na wa kuwa na kichwa chenye mvi, Ee Mungu, usiniache,+Mpaka nikitangazie kizazi habari za mkono wako,+Habari za nguvu zako, kwa wale wote watakaokuja.+ 19  Uadilifu wako, Ee Mungu, unafika kileleni;+Na kuhusu mambo makuu ambayo umeyafanya,+Ee Mungu, ni nani aliye kama wewe?+ 20  Kwa sababu umenifanya nione taabu nyingi na misiba,+Unifufue tena;+Na unipandishe tena kutoka katika vilindi vya maji vya dunia.+ 21  Na uuongeze ukuu wangu,+Na unizingire na kunifariji.+ 22  Mimi pia, nitakusifu kwa chombo cha kinanda,+Kuhusu ukweli wako, Ee Mungu wangu.+Nitakupigia muziki kwa kinubi, Ee Mtakatifu wa Israeli.+ 23  Midomo yangu itapiga vigelegele kwa shangwe wakati wowote ninapokupigia muziki,+Naam, nafsi yangu, ambayo umeikomboa.+ 24  Pia, ulimi wangu mwenyewe, mchana kutwa, utasema juu ya uadilifu wako kwa sauti ya chini,+Kwa maana wameaibika, kwa maana wamefedheheka, wale wanaonitafutia msiba.+

Maelezo ya Chini