Zaburi 71:1-24
71 Nimekukimbilia wewe, Ee Yehova.+Nisiaibike kamwe.+
2 Unikomboe kwa uadilifu wako na kuniokoa.+Tega sikio lako kwangu na uniokoe.+
3 Uwe kwangu ngome ya mwamba ya kuingia ndani daima.+Utoe amri ili kuniokoa,+Kwa maana wewe ni mwamba wangu na ngome yangu.+
4 Ee Mungu wangu, uniokoe na mkono wa mwovu,+Na mkono wa mtu anayetenda kwa njia isiyo ya haki na kwa ukandamizaji.+
5 Kwa maana wewe ni tumaini langu,+ Ee Bwana Mwenye Enzi Kuu, Yehova, tegemeo langu tangu ujana wangu.+
6 Nimekutegemea tangu tumboni;+Wewe ndiye Yule anayenitenganisha na sehemu za ndani za mama yangu.+Sifa yangu kwako ni ya daima.+
7 Nimekuwa kama muujiza kwa watu wengi;+Lakini wewe ni kimbilio langu lenye nguvu.+
8 Kinywa changu kimejawa na sifa zako,+Mchana kutwa na uzuri wako.+
9 Usinitupe wakati wa uzee;+Wakati tu nguvu zangu zinapungua, usiniache.+
10 Kwa maana adui zangu wamesema juu yangu,+Na walewale wanaoitafuta nafsi yangu wameshauriana pamoja,+
11 Wakisema: “Mungu mwenyewe amemwacha.+Mfuatilieni na kumkamata, kwa maana hakuna mkombozi.”+
12 Ee Mungu, usikae mbali nami.+Ee Mungu wangu, ufanye haraka kunisaidia.+
13 Hao na waaibike, hao na wafikie mwisho wao, wanaoshindana na nafsi yangu.+Hao na wajifunike kwa shutuma na fedheha wanaonitafutia msiba.+
14 Lakini mimi, nitangoja daima,+Nami nitaongezea sifa zako zote.
15 Kinywa changu mwenyewe kitasimulia uadilifu wako,+Wokovu wako mchana kutwa,+Kwa maana sijapata kujua hesabu yake.+
16 Nitaingia na nguvu kuu,+ Ee Bwana Mwenye Enzi Kuu+ Yehova;Nitautangaza uadilifu wako, naam, wako peke yako.+
17 Ee Mungu, umenifundisha tangu ujana wangu,+Na mpaka sasa ninaendelea kutangaza kazi zako za ajabu.+
18 Na mpaka wakati wa uzee na wa kuwa na kichwa chenye mvi, Ee Mungu, usiniache,+Mpaka nikitangazie kizazi habari za mkono wako,+Habari za nguvu zako, kwa wale wote watakaokuja.+
19 Uadilifu wako, Ee Mungu, unafika kileleni;+Na kuhusu mambo makuu ambayo umeyafanya,+Ee Mungu, ni nani aliye kama wewe?+
20 Kwa sababu umenifanya nione taabu nyingi na misiba,+Unifufue tena;+Na unipandishe tena kutoka katika vilindi vya maji vya dunia.+
21 Na uuongeze ukuu wangu,+Na unizingire na kunifariji.+
22 Mimi pia, nitakusifu kwa chombo cha kinanda,+Kuhusu ukweli wako, Ee Mungu wangu.+Nitakupigia muziki kwa kinubi, Ee Mtakatifu wa Israeli.+
23 Midomo yangu itapiga vigelegele kwa shangwe wakati wowote ninapokupigia muziki,+Naam, nafsi yangu, ambayo umeikomboa.+
24 Pia, ulimi wangu mwenyewe, mchana kutwa, utasema juu ya uadilifu wako kwa sauti ya chini,+Kwa maana wameaibika, kwa maana wamefedheheka, wale wanaonitafutia msiba.+