Zaburi 100:1-5

Muziki wa kutoa shukrani.+ 100  Mpigieni Yehova kelele za ushindi, enyi nyote watu wa dunia.+   Mtumikieni Yehova kwa kushangilia.+Njooni mbele zake kwa vigelegele vya shangwe.+   Jueni kwamba Yehova ni Mungu.+Yeye ndiye aliyetufanya, wala si sisi wenyewe.+Sisi ni watu wake na kondoo wa malisho yake.+   Ingieni katika malango yake mkiwa na shukrani,+Katika nyua zake mkiwa na sifa.+Mtoleeni shukrani, libarikini jina lake.+   Kwa maana Yehova ni mwema;+Fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo,+Na uaminifu wake ni wa kizazi baada ya kizazi.+

Maelezo ya Chini