Zaburi 100:1-5
Muziki wa kutoa shukrani.+
100 Mpigieni Yehova kelele za ushindi, enyi nyote watu wa dunia.+
2 Mtumikieni Yehova kwa kushangilia.+Njooni mbele zake kwa vigelegele vya shangwe.+
3 Jueni kwamba Yehova ni Mungu.+Yeye ndiye aliyetufanya, wala si sisi wenyewe.+Sisi ni watu wake na kondoo wa malisho yake.+
4 Ingieni katika malango yake mkiwa na shukrani,+Katika nyua zake mkiwa na sifa.+Mtoleeni shukrani, libarikini jina lake.+
5 Kwa maana Yehova ni mwema;+Fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo,+Na uaminifu wake ni wa kizazi baada ya kizazi.+