Zaburi 102:1-28

Sala ya mwenye kuteseka ikiwa atakuwa mnyonge na kumwaga hangaiko lake mbele za Yehova.+ 102  Ee Yehova, uisikie sala yangu;+Na kilio changu mwenyewe cha kuomba msaada na kije kwako.+   Usinifiche uso wako siku nitakayokuwa katika dhiki kali.+Utege sikio lako kwangu;+Siku nitakayoita, ufanye haraka, unijibu.+   Kwa maana siku zangu zimefikia mwisho kama moshi,+Na mifupa yangu imefanywa kuwa na moto mkali kama jiko.+   Moyo wangu umepigwa kama majani nao umekauka,+Kwa maana nimesahau kula chakula changu.+   Kwa sababu ya sauti ya kuugua kwangu+Mifupa yangu imeshikamana na nyama yangu.+   Nafanana na mwari wa jangwani.+Nimekuwa kama bundi mdogo wa mahali palipofanywa ukiwa.   Nimekonda,Nami nimekuwa kama ndege aliye peke yake juu ya dari.+   Adui zangu wamenishutumu mchana kutwa.+Wale wanaonifanya mpumbavu hata wameapa kwa jina langu.+   Kwa maana nimekula majivu kama mkate;+Navyo vitu ninavyokunywa nimevichanganya hata pamoja na kulia,+ 10  Kwa sababu ya shutuma zako na kuudhika kwako;+Kwa maana umeniinua, ili unitupilie mbali.+ 11  Siku zangu ni kama kivuli ambacho kimepungua,+nami mwenyewe nimekauka kama majani tu.+ 12  Lakini wewe, Ee Yehova, utakaa mpaka wakati usio na kipimo,+Na ukumbusho wako utakuwa kwa kizazi baada ya kizazi.+ 13  Wewe mwenyewe utasimama, utakuwa na rehema juu ya Sayuni,+Kwa maana ni majira ya kumwonyesha kibali,Kwa maana wakati uliowekwa umefika.+ 14  Kwa maana watumishi wako wamepata raha katika mawe yake+Nao wanaelekeza kibali chao kwenye mavumbi yake.+ 15  Nayo mataifa yataogopa jina la Yehova,+Na wafalme wote wa dunia utukufu wako.+ 16  Kwa maana hakika Yehova atajenga Sayuni;+Lazima ataonekana katika utukufu wake.+ 17  Hakika ataielekea sala ya wale waliovuliwa kila kitu,+Naye hataidharau sala yao.+ 18  Hili limeandikwa kwa ajili ya kizazi cha wakati ujao;+Na watu watakaoumbwa watamsifu Yah.+ 19  Kwa maana yeye ametazama chini kutoka katika kilele chake kitakatifu,+Kutoka katika mbingu Yehova ametazama chini, naam, kwenye dunia,+ 20  Ili kusikia kuugua kwa mfungwa,+Ili kuwafungua wale waliowekwa kwa ajili ya kifo;+ 21  Ili jina la Yehova litangazwe katika Sayuni+Na sifa yake katika Yerusalemu,+ 22  Vikundi vya watu vitakapokusanywa vyote pamoja,+Na falme ili kumtumikia Yehova.+ 23  Alizitesa nguvu zangu njiani,+Alizifupisha siku zangu.+ 24  Nikasema: “Ee Mungu wangu,Usiniondoe katikati ya siku zangu;+Miaka yako ni ya vizazi vyote.+ 25  Wewe uliiweka misingi ya dunia zamani za kale,+Nazo mbingu ni kazi ya mikono yako.+ 26  Hizo zitaangamia, lakini wewe mwenyewe utaendelea kusimama;+Nazo zote zitachakaa kama vazi.+Utazibadili kama mavazi, nazo zitamaliza zamu yake.+ 27  Lakini wewe ni yuleyule, nayo miaka yako mwenyewe haitamalizika.+ 28  Wana wa watumishi wako wataendelea kukaa;+Na mbele zako uzao wao utafanywa imara.”+

Maelezo ya Chini