Zaburi 102:1-28
Sala ya mwenye kuteseka ikiwa atakuwa mnyonge na kumwaga hangaiko lake mbele za Yehova.+
102 Ee Yehova, uisikie sala yangu;+Na kilio changu mwenyewe cha kuomba msaada na kije kwako.+
2 Usinifiche uso wako siku nitakayokuwa katika dhiki kali.+Utege sikio lako kwangu;+Siku nitakayoita, ufanye haraka, unijibu.+
3 Kwa maana siku zangu zimefikia mwisho kama moshi,+Na mifupa yangu imefanywa kuwa na moto mkali kama jiko.+
4 Moyo wangu umepigwa kama majani nao umekauka,+Kwa maana nimesahau kula chakula changu.+
5 Kwa sababu ya sauti ya kuugua kwangu+Mifupa yangu imeshikamana na nyama yangu.+
6 Nafanana na mwari wa jangwani.+Nimekuwa kama bundi mdogo wa mahali palipofanywa ukiwa.
7 Nimekonda,Nami nimekuwa kama ndege aliye peke yake juu ya dari.+
8 Adui zangu wamenishutumu mchana kutwa.+Wale wanaonifanya mpumbavu hata wameapa kwa jina langu.+
9 Kwa maana nimekula majivu kama mkate;+Navyo vitu ninavyokunywa nimevichanganya hata pamoja na kulia,+
10 Kwa sababu ya shutuma zako na kuudhika kwako;+Kwa maana umeniinua, ili unitupilie mbali.+
11 Siku zangu ni kama kivuli ambacho kimepungua,+nami mwenyewe nimekauka kama majani tu.+
12 Lakini wewe, Ee Yehova, utakaa mpaka wakati usio na kipimo,+Na ukumbusho wako utakuwa kwa kizazi baada ya kizazi.+
13 Wewe mwenyewe utasimama, utakuwa na rehema juu ya Sayuni,+Kwa maana ni majira ya kumwonyesha kibali,Kwa maana wakati uliowekwa umefika.+
14 Kwa maana watumishi wako wamepata raha katika mawe yake+Nao wanaelekeza kibali chao kwenye mavumbi yake.+
15 Nayo mataifa yataogopa jina la Yehova,+Na wafalme wote wa dunia utukufu wako.+
16 Kwa maana hakika Yehova atajenga Sayuni;+Lazima ataonekana katika utukufu wake.+
17 Hakika ataielekea sala ya wale waliovuliwa kila kitu,+Naye hataidharau sala yao.+
18 Hili limeandikwa kwa ajili ya kizazi cha wakati ujao;+Na watu watakaoumbwa watamsifu Yah.+
19 Kwa maana yeye ametazama chini kutoka katika kilele chake kitakatifu,+Kutoka katika mbingu Yehova ametazama chini, naam, kwenye dunia,+
20 Ili kusikia kuugua kwa mfungwa,+Ili kuwafungua wale waliowekwa kwa ajili ya kifo;+
21 Ili jina la Yehova litangazwe katika Sayuni+Na sifa yake katika Yerusalemu,+
22 Vikundi vya watu vitakapokusanywa vyote pamoja,+Na falme ili kumtumikia Yehova.+
23 Alizitesa nguvu zangu njiani,+Alizifupisha siku zangu.+
24 Nikasema: “Ee Mungu wangu,Usiniondoe katikati ya siku zangu;+Miaka yako ni ya vizazi vyote.+
25 Wewe uliiweka misingi ya dunia zamani za kale,+Nazo mbingu ni kazi ya mikono yako.+
26 Hizo zitaangamia, lakini wewe mwenyewe utaendelea kusimama;+Nazo zote zitachakaa kama vazi.+Utazibadili kama mavazi, nazo zitamaliza zamu yake.+
27 Lakini wewe ni yuleyule, nayo miaka yako mwenyewe haitamalizika.+
28 Wana wa watumishi wako wataendelea kukaa;+Na mbele zako uzao wao utafanywa imara.”+