Zaburi 4:1-8
Kwa kiongozi wa vinanda.+ Muziki wa Daudi.
4 Ninapoita, unijibu, Ee Mungu wangu mwadilifu.+Katika taabu unifanyie nafasi panaNionyeshe kibali+ na kuisikia sala yangu.
2 Enyi wana wa watu, utukufu+ wangu utatukanwa mpaka wakati gani,Huku mkiendelea kupenda mambo ya upuuzi,Huku mkiendelea kutafuta uwongo? Sela.
3 Basi jueni kwamba hakika Yehova atamtendea mshikamanifu wake kwa njia ya pekee;+Yehova mwenyewe atasikia ninapomwita.+
4 Fadhaikeni, lakini msitende dhambi.+Semeni moyoni mwenu, kitandani mwenu,+ na kunyamaza. Sela.
5 Toeni dhabihu za uadilifu,+Na kumtumaini Yehova.+
6 Kuna wengi wanaosema: “Ni nani atakayetuonyesha mema?”Inua nuru ya uso wako juu yetu,+ Ee Yehova.
7 Hakika wewe utaupa moyo wangu shangwe+Iliyo kubwa kuliko wakati ambapo nafaka yao na divai yao mpya imejaa.+
8 Katika amani nitajilaza na kulala usingizi,+Kwa maana wewe peke yako, Ee Yehova, hunifanya nikae kwa usalama.+