Zaburi 14:1-7

Kwa kiongozi. Ya Daudi. 14  Asiye na akili amesema katika moyo wake:“Hakuna Yehova.”+Wametenda kwa uharibifu,+ wametenda kwa njia yenye kuchukiza katika shughuli zao.Hakuna yeyote anayefanya mema.+   Kutoka mbinguni Yehova amewatazama wana wa binadamu walio chini,+ Ili aone kama kuna yeyote ambaye ana ufahamu, yeyote anayemtafuta Yehova.+   Wote wamegeuka kando,+ wote ni wafisadi kwa njia ileile;+Hakuna yeyote anayefanya mema,+Hakuna hata mmoja.+   Je, hakuna yeyote kati ya wale wanaotenda mambo yenye kuumiza ambaye ana ujuzi,+Wakila watu wangu kama vile ambavyo wamekula mkate?+Hata hawajamwitia Yehova.+   Hapo wao walijawa na hofu kubwa,+Kwa maana Yehova yuko kati ya kizazi cha mwadilifu.+   Shauri la mwenye kuteseka ninyi huliaibisha,Kwa sababu Yehova ni kimbilio lake.+   Laiti wokovu wa Israeli ungetoka Sayuni!+Wakati ambapo Yehova anawakusanya tena mateka wa watu wake,+Yakobo na ashangilie, Israeli na afurahi.+

Maelezo ya Chini