Zaburi 39:1-13

Kwa kiongozi wa Yeduthuni.+ Muziki wa Daudi. 39  Nilisema: “Nitalinda njia zangu+Ili nisiendelee kutenda dhambi kwa ulimi wangu.+Nitaweka lijamu kama mlinzi wa kinywa changu mwenyewe,+Maadamu mtu yeyote mwovu yuko mbele yangu.”+   Nikawa asiyeweza kusema kwa kukaa kimya;+Nikaendelea kulinyamazia lililo jema,+Na kuumia kwangu kukatengwa.   Moyo wangu ukawa na moto ndani yangu;+Wakati wa kuugua kwangu moto ukaendelea kuwaka.Nilisema kwa ulimi wangu:   “Ee Yehova, nijulishe mwisho wangu,+Na kipimo cha siku zangu—ni kipimo gani,+Ili nipate kujua kadiri nilivyo wa muda mfupi.+   Tazama! Umezifanya siku zangu kuwa chache tu;+Na urefu wa maisha yangu si kitu mbele zako.+Kwa kweli kila mtu wa udongo, ingawa anasimama imara, si kitu ila pumzi tu.+ Sela.   Kwa kweli mtu hutembea huku na huku kama kivuli tu.+Kwa kweli wana msukosuko ambao ni ubatili.+Mmoja anarundika vitu wala hajui ni nani atakayevikusanya.+   Na sasa, nimetumainia nini, Ee Yehova? Matarajio yangu yanakuelekea wewe.+   Unikomboe kutoka katika makosa yangu yote.+Usiniweke kama shutuma ya mtu asiye na akili.+   Niliendelea kuwa asiyeweza kusema;+ sikuweza kufungua kinywa changu,+Kwa maana wewe mwenyewe ulichukua hatua.+ 10  Uniondolee pigo lako.+Nimefikia mwisho kwa sababu ya uadui wa mkono wako.+ 11  Umemrekebisha mtu kwa makaripio dhidi ya kosa,+Nawe unakula vitu vyake vyenye kutamanika kama nondo.+Kwa kweli kila mtu wa udongo ni pumzi tu.+ Sela. 12  Uisikie sala yangu, Ee Yehova,Na usikilize kilio changu cha kutaka msaada.+Usikae kimya machozi yangu yanapotoka.+Kwa maana, kwako, mimi ni mkaaji mgeni tu,+Mhamiaji kama vile mababu zangu wote.+ 13  Usinitazame, ili nipate kung’aa+Kabla sijaenda, nisiwepo.”+

Maelezo ya Chini