Zaburi 44:1-26

Kwa kiongozi. Ya wana wa Kora.+ Maskili. 44  Ee Mungu, tumesikia kwa masikio yetu,Mababu zetu wenyewe wametusimulia+Utendaji ambao ulifanya katika siku zao,+Siku za zamani za kale.+   Wewe mwenyewe kwa mkono wako uliwafukuzia mbali mataifa,+Nawe ukawapanda hao badala yao.+Ukavunja vikundi vya mataifa na kuwafukuza.+   Kwa maana hawakuimiliki nchi hiyo kwa upanga wao wenyewe,+Wala wokovu haukuletwa kwa mkono wao wenyewe.+Kwa maana ulikuwa ni mkono wako wa kuume,+ naam, mkono wako na nuru ya uso wako,Kwa sababu ulipendezwa nao.+   Wewe mwenyewe ni Mfalme wangu, Ee Mungu.+Amuru wokovu mkuu kwa ajili ya Yakobo.+   Kupitia wewe tutawasukuma wapinzani wetu;+Katika jina lako tutawakanyagia chini wale wanaosimama dhidi yetu.+   Kwa maana sikuendelea kuutegemea upinde wangu+Wala si upanga wangu uliokuwa ukiniokoa.+   Kwa maana ulituokoa kutoka kwa wapinzani wetu,+Nawe ukawafanya waone aibu wale wanaotuchukia vikali.+   Tutamtolea Mungu sifa mchana kutwa,+Nasi tutalisifu jina lako mpaka wakati usio na kipimo.+ Sela.   Lakini sasa umetutupilia mbali na unaendelea kutufedhehesha,+Wala huendi pamoja na majeshi yetu.+ 10  Wewe unaendelea kutufanya tugeuke kutoka kwa adui zetu,+Na wale wanaotuchukia vikali wamejinyakulia vitu.+ 11  Wewe unatutoa kama kondoo, kama chakula,+Nawe umetutawanya kati ya mataifa.+ 12  Unawauza watu wako kwa bei ndogo sana,+Wala hujapata faida yoyote kwa bei yao. 13  Unatuweka kuwa shutuma kwa jirani zetu,+Kuwa dharau na dhihaka kwa wale wanaotuzunguka pande zote.+ 14  Umetufanya kuwa neno la kimethali kati ya mataifa,+Kuwa kitu cha kutikisiwa kichwa kati ya vikundi vya mataifa.+ 15  Fedheha yangu iko mbele yangu mchana kutwa,Nayo aibu ya uso wangu mwenyewe imenifunika,+ 16  Kwa sababu ya sauti ya mtu anayeshutumu na kusema vibaya,Kwa sababu ya adui na mtu anayejilipizia kisasi.+ 17  Yote hayo ndiyo yametujia, nasi hatujakusahau,+Wala hatujatenda kwa njia ya uwongo katika agano lako.+ 18  Moyo wetu haujageuka nyuma kwa kukosa imani,+Wala hatua za miguu yetu hazitoki katika njia yako.+ 19  Kwa maana umetuponda katika mahali pa mbwa-mwitu,+Nawe unatufunika kwa kivuli kizito.+ 20  Ikiwa tumelisahau jina la Mungu wetu,Au kumnyooshea mungu mgeni mikono yetu,+ 21  Je, Mungu mwenyewe hatachunguza hilo?+Kwa maana yeye anajua siri za moyo.+ 22  Lakini kwa ajili yako tumeuawa mchana kutwa;Tumehesabiwa kuwa kondoo wa kuchinjwa.+ 23  Uamke. Kwa nini unaendelea kulala usingizi, Ee Yehova?+Uamke. Usiendelee kututupilia mbali milele.+ 24  Kwa nini unaendelea kuuficha uso wako?Kwa nini unasahau mateso yetu na ukandamizaji wetu?+ 25  Kwa maana nafsi yetu imeinama chini mavumbini;+Tumbo letu limeshikamana na udongo. 26  Usimame, utusaidie+Na kutukomboa kwa ajili ya fadhili zako zenye upendo.+

Maelezo ya Chini