Zaburi 44:1-26
Kwa kiongozi. Ya wana wa Kora.+ Maskili.
44 Ee Mungu, tumesikia kwa masikio yetu,Mababu zetu wenyewe wametusimulia+Utendaji ambao ulifanya katika siku zao,+Siku za zamani za kale.+
2 Wewe mwenyewe kwa mkono wako uliwafukuzia mbali mataifa,+Nawe ukawapanda hao badala yao.+Ukavunja vikundi vya mataifa na kuwafukuza.+
3 Kwa maana hawakuimiliki nchi hiyo kwa upanga wao wenyewe,+Wala wokovu haukuletwa kwa mkono wao wenyewe.+Kwa maana ulikuwa ni mkono wako wa kuume,+ naam, mkono wako na nuru ya uso wako,Kwa sababu ulipendezwa nao.+
4 Wewe mwenyewe ni Mfalme wangu, Ee Mungu.+Amuru wokovu mkuu kwa ajili ya Yakobo.+
5 Kupitia wewe tutawasukuma wapinzani wetu;+Katika jina lako tutawakanyagia chini wale wanaosimama dhidi yetu.+
6 Kwa maana sikuendelea kuutegemea upinde wangu+Wala si upanga wangu uliokuwa ukiniokoa.+
7 Kwa maana ulituokoa kutoka kwa wapinzani wetu,+Nawe ukawafanya waone aibu wale wanaotuchukia vikali.+
8 Tutamtolea Mungu sifa mchana kutwa,+Nasi tutalisifu jina lako mpaka wakati usio na kipimo.+ Sela.
9 Lakini sasa umetutupilia mbali na unaendelea kutufedhehesha,+Wala huendi pamoja na majeshi yetu.+
10 Wewe unaendelea kutufanya tugeuke kutoka kwa adui zetu,+Na wale wanaotuchukia vikali wamejinyakulia vitu.+
11 Wewe unatutoa kama kondoo, kama chakula,+Nawe umetutawanya kati ya mataifa.+
12 Unawauza watu wako kwa bei ndogo sana,+Wala hujapata faida yoyote kwa bei yao.
13 Unatuweka kuwa shutuma kwa jirani zetu,+Kuwa dharau na dhihaka kwa wale wanaotuzunguka pande zote.+
14 Umetufanya kuwa neno la kimethali kati ya mataifa,+Kuwa kitu cha kutikisiwa kichwa kati ya vikundi vya mataifa.+
15 Fedheha yangu iko mbele yangu mchana kutwa,Nayo aibu ya uso wangu mwenyewe imenifunika,+
16 Kwa sababu ya sauti ya mtu anayeshutumu na kusema vibaya,Kwa sababu ya adui na mtu anayejilipizia kisasi.+
17 Yote hayo ndiyo yametujia, nasi hatujakusahau,+Wala hatujatenda kwa njia ya uwongo katika agano lako.+
18 Moyo wetu haujageuka nyuma kwa kukosa imani,+Wala hatua za miguu yetu hazitoki katika njia yako.+
19 Kwa maana umetuponda katika mahali pa mbwa-mwitu,+Nawe unatufunika kwa kivuli kizito.+
20 Ikiwa tumelisahau jina la Mungu wetu,Au kumnyooshea mungu mgeni mikono yetu,+
21 Je, Mungu mwenyewe hatachunguza hilo?+Kwa maana yeye anajua siri za moyo.+
22 Lakini kwa ajili yako tumeuawa mchana kutwa;Tumehesabiwa kuwa kondoo wa kuchinjwa.+
23 Uamke. Kwa nini unaendelea kulala usingizi, Ee Yehova?+Uamke. Usiendelee kututupilia mbali milele.+
24 Kwa nini unaendelea kuuficha uso wako?Kwa nini unasahau mateso yetu na ukandamizaji wetu?+
25 Kwa maana nafsi yetu imeinama chini mavumbini;+Tumbo letu limeshikamana na udongo.
26 Usimame, utusaidie+Na kutukomboa kwa ajili ya fadhili zako zenye upendo.+