Zaburi 76:1-12
Kwa kiongozi wa vinanda. Muziki. Wa Asafu.+ Wimbo.
76 Mungu anajulikana katika Yuda;+Katika Israeli jina lake ni kuu.+
2 Na maficho yake yako katika Salemu,+Na makao yake katika Sayuni.+
3 Huko alivunja mishale ya upinde inayowaka,+Ngao na upanga na vita.+ Sela.
4 Umefunikwa na nuru, una utukufu kuliko milima ya mawindo.+
5 Wenye nguvu moyoni wameporwa,+Wamesinzia na kulala usingizi,+Wala hakuna hata mmoja wa wanaume mashujaa ambaye ameiona mikono yake.+
6 Kwa sababu ya kemeo lako, Ee Mungu wa Yakobo, mwendesha-gari na farasi pia wamelala usingizi mzito.+
7 Wewe—ni mwenye kuogopesha,+Na ni nani anayeweza kusimama mbele zako kwa sababu ya nguvu za hasira yako?+
8 Kutoka mbinguni ulifanya kesi isikiwe;+Dunia iliogopa na kukaa kimya+
9 Mungu aliposimama kwenye hukumu,+Ili kuokoa wapole wote wa dunia.+ Sela.
10 Kwa maana ghadhabu ya mwanadamu itakusifu;+Utajifunga ghadhabu iliyobaki.
11 Wekeni nadhiri na kumtimizia Yehova Mungu wenu, ninyi nyote mnaomzunguka pande zote.+Na walete zawadi kwa kuogopa.+
12 Atainyenyekeza roho ya viongozi;+Yeye ni mwenye kuogopesha kwa wafalme wa dunia.+