Zaburi 76:1-12

Kwa kiongozi wa vinanda. Muziki. Wa Asafu.+ Wimbo. 76  Mungu anajulikana katika Yuda;+Katika Israeli jina lake ni kuu.+   Na maficho yake yako katika Salemu,+Na makao yake katika Sayuni.+   Huko alivunja mishale ya upinde inayowaka,+Ngao na upanga na vita.+ Sela.   Umefunikwa na nuru, una utukufu kuliko milima ya mawindo.+   Wenye nguvu moyoni wameporwa,+Wamesinzia na kulala usingizi,+Wala hakuna hata mmoja wa wanaume mashujaa ambaye ameiona mikono yake.+   Kwa sababu ya kemeo lako, Ee Mungu wa Yakobo, mwendesha-gari na farasi pia wamelala usingizi mzito.+   Wewe—ni mwenye kuogopesha,+Na ni nani anayeweza kusimama mbele zako kwa sababu ya nguvu za hasira yako?+   Kutoka mbinguni ulifanya kesi isikiwe;+Dunia iliogopa na kukaa kimya+   Mungu aliposimama kwenye hukumu,+Ili kuokoa wapole wote wa dunia.+ Sela. 10  Kwa maana ghadhabu ya mwanadamu itakusifu;+Utajifunga ghadhabu iliyobaki. 11  Wekeni nadhiri na kumtimizia Yehova Mungu wenu, ninyi nyote mnaomzunguka pande zote.+Na walete zawadi kwa kuogopa.+ 12  Atainyenyekeza roho ya viongozi;+Yeye ni mwenye kuogopesha kwa wafalme wa dunia.+

Maelezo ya Chini