Zaburi 96:1-13
96 Mwimbieni Yehova wimbo mpya.+Mwimbieni Yehova, enyi watu wote wa dunia.+
2 Mwimbieni Yehova, libarikini jina lake.+Tangazeni habari njema za wokovu wake siku baada ya siku.+
3 Tangazeni utukufu wake kati ya mataifa,+Kazi zake za ajabu kati ya vikundi vyote vya watu.+
4 Kwa maana Yehova ni mkuu+ na wa kusifiwa sana.Ni mwenye kuogopesha kuliko miungu mingine yote.+
5 Kwa maana miungu yote ya vikundi vya watu ni miungu isiyo na thamani;+Lakini Yehova, amezifanya mbingu.+
6 Utukufu na fahari ziko mbele zake;+Nguvu na uzuri zipo katika patakatifu pake.+
7 Mhesabieni Yehova, enyi familia za vikundi vya watu,+Mhesabieni Yehova utukufu na nguvu.+
8 Mhesabieni Yehova utukufu wa jina lake;+Chukueni zawadi na mwingie katika nyua zake.+
9 Mwinamieni Yehova katika pambo takatifu;+Iweni na maumivu makali kwa sababu yake, enyi nyote watu wa dunia.+
10 Semeni kati ya mataifa: “Yehova amekuwa mfalme.+Nchi yenye kuzaa pia hufanywa imara ili isitikiswe.+Yeye atatetea kwa unyoofu vikundi vya watu katika kesi yao.”+
11 Mbingu na zifurahi, na dunia ishangilie.+Bahari na ingurume na vitu vinavyoijaza.+
12 Nchi na ifurahi na vyote vilivyomo.+Na wakati uleule miti yote ya msituni na ishangilie+
13 Mbele za Yehova. Kwa maana amekuja;+Kwa maana amekuja kuihukumu dunia.+Ataihukumu kwa uadilifu nchi yenye kuzaa+Na vikundi vya watu kwa uaminifu.+