Zaburi 96:1-13

96  Mwimbieni Yehova wimbo mpya.+Mwimbieni Yehova, enyi watu wote wa dunia.+   Mwimbieni Yehova, libarikini jina lake.+Tangazeni habari njema za wokovu wake siku baada ya siku.+   Tangazeni utukufu wake kati ya mataifa,+Kazi zake za ajabu kati ya vikundi vyote vya watu.+   Kwa maana Yehova ni mkuu+ na wa kusifiwa sana.Ni mwenye kuogopesha kuliko miungu mingine yote.+   Kwa maana miungu yote ya vikundi vya watu ni miungu isiyo na thamani;+Lakini Yehova, amezifanya mbingu.+   Utukufu na fahari ziko mbele zake;+Nguvu na uzuri zipo katika patakatifu pake.+   Mhesabieni Yehova, enyi familia za vikundi vya watu,+Mhesabieni Yehova utukufu na nguvu.+   Mhesabieni Yehova utukufu wa jina lake;+Chukueni zawadi na mwingie katika nyua zake.+   Mwinamieni Yehova katika pambo takatifu;+Iweni na maumivu makali kwa sababu yake, enyi nyote watu wa dunia.+ 10  Semeni kati ya mataifa: “Yehova amekuwa mfalme.+Nchi yenye kuzaa pia hufanywa imara ili isitikiswe.+Yeye atatetea kwa unyoofu vikundi vya watu katika kesi yao.”+ 11  Mbingu na zifurahi, na dunia ishangilie.+Bahari na ingurume na vitu vinavyoijaza.+ 12  Nchi na ifurahi na vyote vilivyomo.+Na wakati uleule miti yote ya msituni na ishangilie+ 13  Mbele za Yehova. Kwa maana amekuja;+Kwa maana amekuja kuihukumu dunia.+Ataihukumu kwa uadilifu nchi yenye kuzaa+Na vikundi vya watu kwa uaminifu.+

Maelezo ya Chini