Zaburi 105:1-45

105  Mshukuruni Yehova, liitieni jina lake,+Yajulisheni matendo yake katikati ya vikundi vya watu.+   Mwimbieni, mpigieni muziki,+Jishughulisheni na kazi zake zote za ajabu.+   Jisifuni katika jina lake takatifu.+Moyo wa wale wanaomtafuta Yehova na ushangilie.+   Mtafuteni Yehova na nguvu zake.+Utafuteni uso wake daima.+   Kumbukeni kazi zake za ajabu ambazo amefanya,+Miujiza yake na maamuzi ya hukumu ya kinywa chake,+   Enyi uzao wa Abrahamu mtumishi wake,+Enyi wana wa Yakobo, wachaguliwa wake.+   Yeye ni Yehova Mungu wetu.+Maamuzi yake ya hukumu yako duniani pote.+   Amelikumbuka agano lake mpaka wakati usio na kipimo,+Neno ambalo aliamuru, mpaka vizazi elfu,+   Agano ambalo alifanya na Abrahamu,+Na ahadi yake yenye kiapo aliyomwapia Isaka,+ 10  Kiapo ambacho alikiendeleza kikiwa sharti kwa Yakobo,Kama agano lenye kudumu kwa Israeli mpaka wakati usio na kipimo,+ 11  Akisema: “Nitakupa wewe nchi ya Kanaani+Kuwa fungu la urithi wenu.”+ 12  Huo ni wakati walipokuwa wachache,+Naam, wachache sana, na wakaaji wageni humo.+ 13  Nao wakaendelea kutembea kutoka kwa taifa moja mpaka kwa taifa lingine,+Kutoka katika ufalme mmoja mpaka kwa kikundi kingine cha watu.+ 14  Hakumruhusu binadamu yeyote awapunje,+Bali aliwakaripia wafalme kwa sababu yao,+ 15  Akisema: “Msiwaguse watiwa-mafuta wangu,+Wala msiwatendee manabii wangu lolote lililo baya.”+ 16  Naye akaitisha njaa juu ya nchi;+Alivunja kila fimbo ambayo mikate ya mviringo ilining’inizwa juu yake.+ 17  Akamtuma mtu mbele yao,Ambaye aliuzwa awe mtumwa, Yosefu.+ 18  Wakaitesa miguu yake kwa pingu,+Nafsi yake ikaingia katika vyuma;+ 19  Mpaka wakati neno lake lilipotimia,+Maneno ya Yehova mwenyewe yakamsafisha.+ 20  Mfalme akatuma watu ili apate kumwachilia,+Mtawala wa vikundi vya watu, ili apate kumfungua. 21  Akamweka kuwa bwana wa nyumba yake+Na kuwa mtawala juu ya mali yake yote,+ 22  Ili awafunge wakuu wake kama inavyopenda nafsi yake+Na ili apate kuwafundisha hekima hata wanaume wake wazee.+ 23  Na Israeli akaingia Misri,+Na Yakobo mwenyewe akakaa akiwa mgeni katika nchi ya Hamu.+ 24  Naye akaendelea kuwafanya watu wake wazaane sana,+Na hatua kwa hatua akawafanya kuwa wenye uwezo kuliko adui zao.+ 25  Akaiacha mioyo yao ibadilike ili kuwachukia watu wake,+Ili wajiendeshe kwa ujanja juu ya watumishi wake.+ 26  Alimtuma Musa mtumishi wake,+Haruni aliyekuwa amemchagua.+ 27  Wakaweka kati yao mambo ya ishara zake,+Na miujiza katika nchi ya Hamu.+ 28  Alituma giza na kwa hiyo akafanya kuwe na giza;+Nao hawakuyaasi maneno yake.+ 29  Aliyabadili maji yao yakawa damu,+Akawaua samaki wao.+ 30  Nchi yao ikajaa vyura,+Katika vyumba vya ndani vya wafalme. 31  Alisema mainzi waingie,+Na chawa katika maeneo yao yote.+ 32  Aliifanya mvua yao iwe mvua ya mawe,+Moto wenye mwali juu ya nchi.+ 33  Naye akapiga mizabibu yao na mitini yaoNa kuvunja miti ya eneo lao.+ 34  Akasema nzige waingie,+Na nzige wachanga, wasio na hesabu.+ 35  Nao wakala mimea yote katika nchi yao;+Pia wakala mazao ya udongo wao. 36  Naye akapiga na kuua kila mzaliwa wa kwanza katika nchi yao,+Mwanzo wa nguvu zao zote za uzazi.+ 37  Naye akaanza kuwatoa nje wakiwa na fedha na dhahabu;+Na katikati ya makabila yake hapakuwa na yeyote mwenye kujikwaa. 38  Misri ilishangilia walipoondoka,Kwa maana hofu yao ilikuwa imewaangukia.+ 39  Alitandaza wingu lifunike,+Na moto utoe nuru wakati wa usiku.+ 40  Waliomba, naye akaleta kware,+Na kwa mkate kutoka mbinguni akaendelea kuwashibisha.+ 41  Alifungua mwamba, na maji yakaanza kutiririka;+Nayo yakapita katika maeneo yasiyo na maji kama mto.+ 42  Kwa maana alilikumbuka neno lake takatifu kwa Abrahamu mtumishi wake.+ 43  Kwa hiyo akawatoa watu wake kwa kushangilia,+Wachaguliwa wake kwa vigelegele vya shangwe.+ 44  Na hatua kwa hatua akawapa nchi za mataifa,+Nao wakaendelea kumiliki kazi ngumu ya vikundi vya mataifa,+ 45  Ili wapate kushika masharti yake+Na kushika sheria zake.+Msifuni Yah!+

Maelezo ya Chini