Zaburi 105:1-45
105 Mshukuruni Yehova, liitieni jina lake,+Yajulisheni matendo yake katikati ya vikundi vya watu.+
2 Mwimbieni, mpigieni muziki,+Jishughulisheni na kazi zake zote za ajabu.+
3 Jisifuni katika jina lake takatifu.+Moyo wa wale wanaomtafuta Yehova na ushangilie.+
4 Mtafuteni Yehova na nguvu zake.+Utafuteni uso wake daima.+
5 Kumbukeni kazi zake za ajabu ambazo amefanya,+Miujiza yake na maamuzi ya hukumu ya kinywa chake,+
6 Enyi uzao wa Abrahamu mtumishi wake,+Enyi wana wa Yakobo, wachaguliwa wake.+
7 Yeye ni Yehova Mungu wetu.+Maamuzi yake ya hukumu yako duniani pote.+
8 Amelikumbuka agano lake mpaka wakati usio na kipimo,+Neno ambalo aliamuru, mpaka vizazi elfu,+
9 Agano ambalo alifanya na Abrahamu,+Na ahadi yake yenye kiapo aliyomwapia Isaka,+
10 Kiapo ambacho alikiendeleza kikiwa sharti kwa Yakobo,Kama agano lenye kudumu kwa Israeli mpaka wakati usio na kipimo,+
11 Akisema: “Nitakupa wewe nchi ya Kanaani+Kuwa fungu la urithi wenu.”+
12 Huo ni wakati walipokuwa wachache,+Naam, wachache sana, na wakaaji wageni humo.+
13 Nao wakaendelea kutembea kutoka kwa taifa moja mpaka kwa taifa lingine,+Kutoka katika ufalme mmoja mpaka kwa kikundi kingine cha watu.+
14 Hakumruhusu binadamu yeyote awapunje,+Bali aliwakaripia wafalme kwa sababu yao,+
15 Akisema: “Msiwaguse watiwa-mafuta wangu,+Wala msiwatendee manabii wangu lolote lililo baya.”+
16 Naye akaitisha njaa juu ya nchi;+Alivunja kila fimbo ambayo mikate ya mviringo ilining’inizwa juu yake.+
17 Akamtuma mtu mbele yao,Ambaye aliuzwa awe mtumwa, Yosefu.+
18 Wakaitesa miguu yake kwa pingu,+Nafsi yake ikaingia katika vyuma;+
19 Mpaka wakati neno lake lilipotimia,+Maneno ya Yehova mwenyewe yakamsafisha.+
20 Mfalme akatuma watu ili apate kumwachilia,+Mtawala wa vikundi vya watu, ili apate kumfungua.
21 Akamweka kuwa bwana wa nyumba yake+Na kuwa mtawala juu ya mali yake yote,+
22 Ili awafunge wakuu wake kama inavyopenda nafsi yake+Na ili apate kuwafundisha hekima hata wanaume wake wazee.+
23 Na Israeli akaingia Misri,+Na Yakobo mwenyewe akakaa akiwa mgeni katika nchi ya Hamu.+
24 Naye akaendelea kuwafanya watu wake wazaane sana,+Na hatua kwa hatua akawafanya kuwa wenye uwezo kuliko adui zao.+
25 Akaiacha mioyo yao ibadilike ili kuwachukia watu wake,+Ili wajiendeshe kwa ujanja juu ya watumishi wake.+
26 Alimtuma Musa mtumishi wake,+Haruni aliyekuwa amemchagua.+
27 Wakaweka kati yao mambo ya ishara zake,+Na miujiza katika nchi ya Hamu.+
28 Alituma giza na kwa hiyo akafanya kuwe na giza;+Nao hawakuyaasi maneno yake.+
29 Aliyabadili maji yao yakawa damu,+Akawaua samaki wao.+
30 Nchi yao ikajaa vyura,+Katika vyumba vya ndani vya wafalme.
31 Alisema mainzi waingie,+Na chawa katika maeneo yao yote.+
32 Aliifanya mvua yao iwe mvua ya mawe,+Moto wenye mwali juu ya nchi.+
33 Naye akapiga mizabibu yao na mitini yaoNa kuvunja miti ya eneo lao.+
34 Akasema nzige waingie,+Na nzige wachanga, wasio na hesabu.+
35 Nao wakala mimea yote katika nchi yao;+Pia wakala mazao ya udongo wao.
36 Naye akapiga na kuua kila mzaliwa wa kwanza katika nchi yao,+Mwanzo wa nguvu zao zote za uzazi.+
37 Naye akaanza kuwatoa nje wakiwa na fedha na dhahabu;+Na katikati ya makabila yake hapakuwa na yeyote mwenye kujikwaa.
38 Misri ilishangilia walipoondoka,Kwa maana hofu yao ilikuwa imewaangukia.+
39 Alitandaza wingu lifunike,+Na moto utoe nuru wakati wa usiku.+
40 Waliomba, naye akaleta kware,+Na kwa mkate kutoka mbinguni akaendelea kuwashibisha.+
41 Alifungua mwamba, na maji yakaanza kutiririka;+Nayo yakapita katika maeneo yasiyo na maji kama mto.+
42 Kwa maana alilikumbuka neno lake takatifu kwa Abrahamu mtumishi wake.+
43 Kwa hiyo akawatoa watu wake kwa kushangilia,+Wachaguliwa wake kwa vigelegele vya shangwe.+
44 Na hatua kwa hatua akawapa nchi za mataifa,+Nao wakaendelea kumiliki kazi ngumu ya vikundi vya mataifa,+
45 Ili wapate kushika masharti yake+Na kushika sheria zake.+Msifuni Yah!+