Zaburi 128:1-6

Wimbo wa Mipando. 128  Mwenye furaha ni kila mtu anayemwogopa Yehova.+Anayetembea katika njia zake.+   Kwa maana utakula kazi ngumu ya mikono yako mwenyewe.+Utakuwa mwenye furaha na mambo yatakwendea vema.+   Mke wako atakuwa kama mzabibu unaozaa matunda+Katika sehemu za ndani kabisa za nyumba yako.Wana wako watakuwa kama miche ya mizeituni+ kuizunguka meza yako pande zote.   Tazama! Hivyo ndivyo atakavyobarikiwa mwanamume+Anayemwogopa Yehova.+   Yehova atakubariki kutoka Sayuni.+Uone pia uzuri wa Yerusalemu siku zote za maisha yako.+   Na uone wana wa wana wako.+Na kuwe na amani juu ya Israeli.+

Maelezo ya Chini