Zaburi 128:1-6
Wimbo wa Mipando.
128 Mwenye furaha ni kila mtu anayemwogopa Yehova.+Anayetembea katika njia zake.+
2 Kwa maana utakula kazi ngumu ya mikono yako mwenyewe.+Utakuwa mwenye furaha na mambo yatakwendea vema.+
3 Mke wako atakuwa kama mzabibu unaozaa matunda+Katika sehemu za ndani kabisa za nyumba yako.Wana wako watakuwa kama miche ya mizeituni+ kuizunguka meza yako pande zote.
4 Tazama! Hivyo ndivyo atakavyobarikiwa mwanamume+Anayemwogopa Yehova.+
5 Yehova atakubariki kutoka Sayuni.+Uone pia uzuri wa Yerusalemu siku zote za maisha yako.+
6 Na uone wana wa wana wako.+Na kuwe na amani juu ya Israeli.+