Zaburi 16:1-11
Miktamu ya Daudi.
16 Unihifadhi, Ee Mungu, kwa maana nimekukimbilia wewe.+
2 Nimemwambia Yehova: “Wewe ni Yehova; wema wangu si kwa ajili yako,+
3 Bali kwa watakatifu walio duniani.Wao, naam, wale mashuhuri, ndio ninaopendezwa nao kabisa.”+
4 Maumivu huwa mengi kwa wale ambao, wakati kuna mtu mwingine, humfuata haraka.+Sitamimina matoleo yao ya kinywaji ya damu,+Nami sitayachukua majina yao juu ya midomo yangu.+
5 Yehova ndiye sehemu ya fungu langu+ nililogawiwa na ya kikombe changu.+Wewe unaishika sana kura yangu.
6 Kamba za kupimia zimeniangukia mahali panapopendeza.+Kwa kweli, miliki yangu mwenyewe naikubali.
7 Nitambariki Yehova, ambaye amenipa shauri.+Kwa kweli, nyakati za usiku figo zangu zimenirekebisha.+
8 Nimemweka Yehova mbele yangu daima.+Kwa sababu yuko upande wa mkono wangu wa kuume, sitatikiswa.+
9 Kwa hiyo moyo wangu unashangilia, nao utukufu wangu una mwelekeo wa kuwa na shangwe.+Pia, mwili wangu mwenyewe utakaa katika usalama.+
10 Kwa maana hutaiacha nafsi yangu katika Kaburi.*+Hutamruhusu mshikamanifu wako aone shimo.+
11 Utanijulisha njia ya uzima.+Shangwe ya kutosha iko pamoja na uso wako;+Kuna uzuri upande wa mkono wako wa kuume milele.+
Maelezo ya Chini
^ Sheoli. Tazama Nyongeza 4.