Zaburi 16:1-11

Miktamu ya Daudi. 16  Unihifadhi, Ee Mungu, kwa maana nimekukimbilia wewe.+   Nimemwambia Yehova: “Wewe ni Yehova; wema wangu si kwa ajili yako,+   Bali kwa watakatifu walio duniani.Wao, naam, wale mashuhuri, ndio ninaopendezwa nao kabisa.”+   Maumivu huwa mengi kwa wale ambao, wakati kuna mtu mwingine, humfuata haraka.+Sitamimina matoleo yao ya kinywaji ya damu,+Nami sitayachukua majina yao juu ya midomo yangu.+   Yehova ndiye sehemu ya fungu langu+ nililogawiwa na ya kikombe changu.+Wewe unaishika sana kura yangu.   Kamba za kupimia zimeniangukia mahali panapopendeza.+Kwa kweli, miliki yangu mwenyewe naikubali.   Nitambariki Yehova, ambaye amenipa shauri.+Kwa kweli, nyakati za usiku figo zangu zimenirekebisha.+   Nimemweka Yehova mbele yangu daima.+Kwa sababu yuko upande wa mkono wangu wa kuume, sitatikiswa.+   Kwa hiyo moyo wangu unashangilia, nao utukufu wangu una mwelekeo wa kuwa na shangwe.+Pia, mwili wangu mwenyewe utakaa katika usalama.+ 10  Kwa maana hutaiacha nafsi yangu katika Kaburi.*+Hutamruhusu mshikamanifu wako aone shimo.+ 11  Utanijulisha njia ya uzima.+Shangwe ya kutosha iko pamoja na uso wako;+Kuna uzuri upande wa mkono wako wa kuume milele.+

Maelezo ya Chini

Sheoli. Tazama Nyongeza 4.