Zaburi 108:1-13
Wimbo. Muziki wa Daudi.
108 Ee Mungu, moyo wangu uko imara.+Nitaimba na kupiga muziki,+Naam, utukufu wangu.+
2 Amka, Ee kinanda; nawe pia, Ee kinubi.+Nitayaamsha mapambazuko.+
3 Nitakusifu katikati ya vikundi vya watu, Ee Yehova;+Nami nitakupigia muziki katikati ya vikundi vya mataifa+
4 Kwa maana fadhili zako zenye upendo ni kuu mpaka mbinguni,+Na ukweli wako mpaka angani.+
5 Utukuzwe juu ya mbingu, Ee Mungu;+Na utukufu wako na uwe juu ya dunia yote.+
6 Ili wapendwa wako waokolewe,+Ee, uokoe kwa mkono wako wa kuume na kunijibu.+
7 Mungu mwenyewe amesema katika utakatifu wake:+“Nitashangilia, nitamgawanya Shekemu+ awe fungu;+Na nchi tambarare ya chini ya Sukothi+ nitaipima.
8 Gileadi+ ni yangu; Manase+ ni yangu;Na Efraimu ni ngome ya aliye mkuu wangu;+Yuda ni fimbo yangu ya kiongozi.+
9 Moabu+ ni chungu changu cha kuoshea.+Nitatupa kiatu+ changu juu ya Edomu.+Nitapiga kelele za ushindi+ juu ya Ufilisti.”+
10 Ni nani atakayenipeleka kwenye jiji lenye ngome?+Ni nani ambaye kwa kweli ataniongoza mpaka Edomu?+
11 Je, si wewe, Ee Mungu ambaye umetutupilia mbali+Na ambaye huendi pamoja na majeshi yetu ukiwa Mungu?+
12 Utusaidie kutokana na taabu,+Kwa maana wokovu wa mtu wa udongo haufai kitu.+
13 Mungu atatuwezesha kupata nguvu,+Na yeye mwenyewe atawakanyagia chini wapinzani wetu.+