Zaburi 61:1-8

Kwa kiongozi wa vinanda. Ya Daudi. 61  Ee Mungu, usikie kilio changu cha kusihi.+Uisikilize sala yangu.+   Kutoka mwisho wa dunia nitakulilia wewe, naam, wewe, moyo wangu unapokuwa mnyonge.+Uniongoze kwenye mwamba ambao uko juu kuliko mimi.+   Kwa maana umekuwa kimbilio langu,+Mnara wenye nguvu mbele ya uso wa adui.+   Nitakuwa mgeni katika hema lako mpaka nyakati zisizo nakipimo;+Nitakimbilia maficho ya mabawa yako.+ Sela.   Kwa maana wewe mwenyewe, Ee Mungu, umesikiliza nadhiri zangu.+Umenipa urithi wa wale wanaoliogopa jina lako.+   Utaongeza siku kwenye siku za mfalme;+Miaka yake itakuwa kama kizazi baada ya kizazi.+   Atakaa mpaka wakati usio na kipimo mbele za Mungu;+Uagize fadhili zenye upendo na ukweli, ili zipate kumlinda.+   Kwa hiyo jina lako nitalipigia muziki milele,+Ili nipate kutimiza nadhiri zangu siku baada ya siku.+

Maelezo ya Chini