Zaburi 61:1-8
Kwa kiongozi wa vinanda. Ya Daudi.
61 Ee Mungu, usikie kilio changu cha kusihi.+Uisikilize sala yangu.+
2 Kutoka mwisho wa dunia nitakulilia wewe, naam, wewe, moyo wangu unapokuwa mnyonge.+Uniongoze kwenye mwamba ambao uko juu kuliko mimi.+
3 Kwa maana umekuwa kimbilio langu,+Mnara wenye nguvu mbele ya uso wa adui.+
4 Nitakuwa mgeni katika hema lako mpaka nyakati zisizo nakipimo;+Nitakimbilia maficho ya mabawa yako.+ Sela.
5 Kwa maana wewe mwenyewe, Ee Mungu, umesikiliza nadhiri zangu.+Umenipa urithi wa wale wanaoliogopa jina lako.+
6 Utaongeza siku kwenye siku za mfalme;+Miaka yake itakuwa kama kizazi baada ya kizazi.+
7 Atakaa mpaka wakati usio na kipimo mbele za Mungu;+Uagize fadhili zenye upendo na ukweli, ili zipate kumlinda.+
8 Kwa hiyo jina lako nitalipigia muziki milele,+Ili nipate kutimiza nadhiri zangu siku baada ya siku.+