Zaburi 142:1-7
Maskili. Ya Daudi, alipokuwa pangoni.+ Sala.
142 Kwa sauti yangu, nilimwomba Yehova msaada;+Kwa sauti yangu, nilianza kumlilia Yehova anionyeshe kibali.+
2 Mbele zake niliendelea kumwaga hangaiko langu;+Mbele zake niliendelea kutangaza juu ya taabu yangu mwenyewe,+
3 Roho+ yangu ilipozimia ndani yangu.Ndipo wewe mwenyewe ulipoijua barabara yangu.+Katika njia ambayo mimi hutembea+Wametega mtego kwa ajili yangu.+
4 Tazama kwenye mkono wa kuume uoneKwamba hakuna yeyote anayenitambua mimi.+Mahali pangu pa kukimbilia pameangamia;+Hakuna yeyote anayeuliza habari za nafsi yangu.+
5 Nilikuitia wewe, Ee Yehova, kwa ajili ya msaada.+Nikasema: “Wewe ni kimbilio langu,+Fungu+ langu katika nchi ya walio hai.”+
6 Usikilize kilio changu cha kusihi,+Kwa maana nimekuwa maskini sana.+Unikomboe kutoka kwa watesaji wangu,+Kwa maana wana nguvu kuliko mimi.+
7 Uitoe nafsi yangu kutoka katika gereza la shimoni+Ili kulisifu jina lako.+Waadilifu na wakusanyike kunizunguka,+Kwa sababu unanitendea inavyofaa.+