Zaburi 142:1-7

Maskili. Ya Daudi, alipokuwa pangoni.+ Sala. 142  Kwa sauti yangu, nilimwomba Yehova msaada;+Kwa sauti yangu, nilianza kumlilia Yehova anionyeshe kibali.+   Mbele zake niliendelea kumwaga hangaiko langu;+Mbele zake niliendelea kutangaza juu ya taabu yangu mwenyewe,+   Roho+ yangu ilipozimia ndani yangu.Ndipo wewe mwenyewe ulipoijua barabara yangu.+Katika njia ambayo mimi hutembea+Wametega mtego kwa ajili yangu.+   Tazama kwenye mkono wa kuume uoneKwamba hakuna yeyote anayenitambua mimi.+Mahali pangu pa kukimbilia pameangamia;+Hakuna yeyote anayeuliza habari za nafsi yangu.+   Nilikuitia wewe, Ee Yehova, kwa ajili ya msaada.+Nikasema: “Wewe ni kimbilio langu,+Fungu+ langu katika nchi ya walio hai.”+   Usikilize kilio changu cha kusihi,+Kwa maana nimekuwa maskini sana.+Unikomboe kutoka kwa watesaji wangu,+Kwa maana wana nguvu kuliko mimi.+   Uitoe nafsi yangu kutoka katika gereza la shimoni+Ili kulisifu jina lako.+Waadilifu na wakusanyike kunizunguka,+Kwa sababu unanitendea inavyofaa.+

Maelezo ya Chini