Zaburi 34:1-22

Ya Daudi, alipokuwa akijifanya mwenda-wazimu+ mbele ya Abimeleki, hivi kwamba akamfukuza, naye akaenda zake. א [ʼAʹleph] 34  Nitambariki Yehova nyakati zote;+Daima sifa yake itakuwa katika kinywa changu.+ ב [Behth]   Nafsi yangu itajisifu katika Yehova;+Wapole watasikia na kushangilia.+ ג [Giʹmel]   Mtukuzeni Yehova pamoja nami,+Na tulikweze jina lake pamoja.+ ד [Daʹleth]   Nilimuuliza Yehova, naye akanijibu,+Naye akanikomboa kutoka katika mambo yote yenye kuniogopesha.+ ה [Heʼ]   Walimtazama, wakang’aa,+Nazo nyuso zao hazingeweza kuona haya kamwe.+ ז [Zaʹyin]   Huyu mwenye kuteseka aliita, na Yehova mwenyewe akasikia.+Na Yeye akamwokoa kutoka katika taabu zake zote.+ ח [Chehth]   Malaika wa Yehova anapiga kambi pande zote kuwazunguka wanaomwogopa,+Na yeye huwaokoa.+ ט [Tehth]   Onjeni mwone ya kuwa Yehova ni mwema;+Mwenye furaha ni mwanamume ambaye humkimbilia.+ י [Yohdh]   Mwogopeni Yehova, enyi watakatifu wake,+Kwa maana wale wanaomwogopa hawakosi chochote.+ כ [Kaph] 10  Wana-simba wenye manyoya shingoni wamekuwa na vichache na kukaa njaa;+Lakini kwa wale wanaomtafuta Yehova, hawatakosa chochote chema.+ ל [Laʹmedh] 11  Njooni, enyi wana, nisikilizeni;+Nitawafundisha kumwogopa Yehova.+ מ [Mem] 12  Ni nani mtu yule anayependezwa na uhai,+Ambaye anapenda siku za kutosha ili kuona mema?+ נ [Nun] 13  Linda ulimi wako na yaliyo mabaya,+Na midomo yako isiseme udanganyifu.+ ס [Saʹmekh] 14  Geuka kutoka katika yaliyo mabaya, na kufanya yaliyo mema;+Utafute amani, na kuifuatia.+ ע [ʽAʹyin] 15  Macho ya Yehova yanawaelekea waadilifu,+Na masikio yake yanakielekea kilio chao cha kuomba msaada.+ פ [Peʼ] 16  Uso wa Yehova uko dhidi ya wale wanaotenda yaliyo mabaya,+Ili kumbukumbu lao liondolewe mbali duniani.+ צ [Tsa·dhehʹ] 17  Wao walilia kwa sauti, naye Yehova mwenyewe akasikia,+Naye akawakomboa kutoka katika taabu zao zote.+ ק [Qohph] 18  Yehova yuko karibu na wale waliovunjika moyo;+Naye huwaokoa wale waliopondwa roho.+ ר [Rehsh] 19  Mwadilifu ana misiba mingi,+Lakini Yehova humkomboa kutoka katika yote hiyo.+ ש [Shin] 20  Yeye anailinda mifupa yote ya mtu huyo;Hakuna hata mmoja uliovunjwa.+ ת [Taw] 21  Msiba utamuua mwovu;+Na wale wanaomchukia mwadilifu watahesabiwa kuwa na hatia.+ 22  Yehova anaikomboa nafsi ya watumishi wake;+Wala hakuna yeyote kati ya wale wanaomkimbilia atakayehesabiwa kuwa na hatia.+

Maelezo ya Chini