Zaburi 34:1-22
Ya Daudi, alipokuwa akijifanya mwenda-wazimu+ mbele ya Abimeleki, hivi kwamba akamfukuza, naye akaenda zake.
א [ʼAʹleph]
34 Nitambariki Yehova nyakati zote;+Daima sifa yake itakuwa katika kinywa changu.+
ב [Behth]
2 Nafsi yangu itajisifu katika Yehova;+Wapole watasikia na kushangilia.+
ג [Giʹmel]
3 Mtukuzeni Yehova pamoja nami,+Na tulikweze jina lake pamoja.+
ד [Daʹleth]
4 Nilimuuliza Yehova, naye akanijibu,+Naye akanikomboa kutoka katika mambo yote yenye kuniogopesha.+
ה [Heʼ]
5 Walimtazama, wakang’aa,+Nazo nyuso zao hazingeweza kuona haya kamwe.+
ז [Zaʹyin]
6 Huyu mwenye kuteseka aliita, na Yehova mwenyewe akasikia.+Na Yeye akamwokoa kutoka katika taabu zake zote.+
ח [Chehth]
7 Malaika wa Yehova anapiga kambi pande zote kuwazunguka wanaomwogopa,+Na yeye huwaokoa.+
ט [Tehth]
8 Onjeni mwone ya kuwa Yehova ni mwema;+Mwenye furaha ni mwanamume ambaye humkimbilia.+
י [Yohdh]
9 Mwogopeni Yehova, enyi watakatifu wake,+Kwa maana wale wanaomwogopa hawakosi chochote.+
כ [Kaph]
10 Wana-simba wenye manyoya shingoni wamekuwa na vichache na kukaa njaa;+Lakini kwa wale wanaomtafuta Yehova, hawatakosa chochote chema.+
ל [Laʹmedh]
11 Njooni, enyi wana, nisikilizeni;+Nitawafundisha kumwogopa Yehova.+
מ [Mem]
12 Ni nani mtu yule anayependezwa na uhai,+Ambaye anapenda siku za kutosha ili kuona mema?+
נ [Nun]
13 Linda ulimi wako na yaliyo mabaya,+Na midomo yako isiseme udanganyifu.+
ס [Saʹmekh]
14 Geuka kutoka katika yaliyo mabaya, na kufanya yaliyo mema;+Utafute amani, na kuifuatia.+
ע [ʽAʹyin]
15 Macho ya Yehova yanawaelekea waadilifu,+Na masikio yake yanakielekea kilio chao cha kuomba msaada.+
פ [Peʼ]
16 Uso wa Yehova uko dhidi ya wale wanaotenda yaliyo mabaya,+Ili kumbukumbu lao liondolewe mbali duniani.+
צ [Tsa·dhehʹ]
17 Wao walilia kwa sauti, naye Yehova mwenyewe akasikia,+Naye akawakomboa kutoka katika taabu zao zote.+
ק [Qohph]
18 Yehova yuko karibu na wale waliovunjika moyo;+Naye huwaokoa wale waliopondwa roho.+
ר [Rehsh]
19 Mwadilifu ana misiba mingi,+Lakini Yehova humkomboa kutoka katika yote hiyo.+
ש [Shin]
20 Yeye anailinda mifupa yote ya mtu huyo;Hakuna hata mmoja uliovunjwa.+
ת [Taw]
21 Msiba utamuua mwovu;+Na wale wanaomchukia mwadilifu watahesabiwa kuwa na hatia.+
22 Yehova anaikomboa nafsi ya watumishi wake;+Wala hakuna yeyote kati ya wale wanaomkimbilia atakayehesabiwa kuwa na hatia.+