Zaburi 53:1-6
Kwa kiongozi juu ya Mahalathi.+ Maskili. Ya Daudi.
53 Asiye na akili amesema katika moyo wake:“Hakuna Yehova.”+Wametenda kwa uharibifu na kutenda kwa njia yenye kuchukiza katika ukosefu wa uadilifu;+Hakuna yeyote anayefanya mema.+
2 Kutoka mbinguni Mungu amewatazama wana wa binadamu walio chini,+Aone kama kuna yeyote ambaye ana ufahamu, yeyote anayemtafuta Yehova.+
3 Wote wamegeuka nyuma, wote ni wafisadi katika njia ileile;+Hakuna yeyote anayefanya mema,+Hakuna hata mmoja.
4 Je, hakuna yeyote kati ya wale wanaotenda mambo yenye kuumiza ambaye ana ujuzi,+Wakila watu wangu kama vile ambavyo wamekula mkate?+Hata hawajamwitia Yehova.+
5 Hapo wamejawa na hofu kubwa,+Mahali ambapo hapakuwa na kitu chenye kutia hofu;+Kwa maana hakika Mungu ataitawanya mifupa ya mtu yeyote anayepiga kambi dhidi yako.+Hakika utawafanya waone aibu, kwa maana Yehova mwenyewe amewakataa.+
6 Laiti wokovu mkuu wa Israeli ungetoka Sayuni!+Wakati ambapo Yehova anawakusanya tena mateka wa watu wake,+Yakobo na ashangilie, Israeli na afurahi.+