Zaburi 98:1-9
Muziki.
98 Mwimbieni Yehova wimbo mpya,+Kwa maana ametenda mambo ya ajabu.+Mkono wake wa kuume, naam, mkono wake mtakatifu, umempatia wokovu.+
2 Yehova amefanya wokovu wake ujulikane;+Ameufunua uadilifu wake machoni pa mataifa.+
3 Amezikumbuka fadhili zake zenye upendo na uaminifu wake kwa nyumba ya Israeli.+Miisho yote ya dunia imeuona wokovu wa Mungu wetu.+
4 Mpigieni Yehova kelele za ushindi, enyi nyote watu wa dunia.+Changamkeni na kupiga vigelegele kwa shangwe na kupiga muziki.+
5 Mpigieni Yehova muziki kwa kinubi,+Kwa kinubi na sauti ya muziki.+
6 Kwa tarumbeta na mvumo wa baragumu+Pigeni kelele za ushindi mbele za Mfalme, Yehova.
7 Bahari na ingurume na vyote vinavyoijaza,+Nchi yenye kuzaa na wanaokaa humo.+
8 Mito na ipige makofi;Milima yote pamoja na ipige vigelegele kwa shangwe+
9 Mbele za Yehova, kwa maana amekuja kuihukumu dunia.+Ataihukumu nchi yenye kuzaa kwa uadilifu+Na vikundi vya watu kwa unyoofu.+