Zaburi 127:1-5

Wimbo wa Mipando. Wa Sulemani. 127  Yehova mwenyewe asipoijenga nyumba,+Ni bure kwamba wajenzi wake wameifanyia kazi ngumu.+Yehova mwenyewe asipolilinda jiji,+Ni bure kwamba mlinzi ameendelea kukaa macho.+   Ni kazi ya bure kwamba ninyi mnaamka mapema,+Kwamba mnakaa mpaka kuchelewa,+Kwamba mnakula chakula kwa maumivu.+Hivi ndivyo anavyompa hata mpendwa wake usingizi.+   Tazama! Wana ni urithi kutoka kwa Yehova;+Uzao wa tumbo ni thawabu.+   Kama mishale mkononi mwa mwanamume mwenye nguvu,+Ndivyo walivyo wana wa ujanani.+   Mwenye furaha ni mwanamume ambaye amelijaza+ podo lake na hao.Hawataona aibu,+Kwa maana wataongea na adui langoni.

Maelezo ya Chini