Zaburi 122:1-9

Wimbo wa Mipando. Wa Daudi. 122  Nilishangilia walipokuwa wakiniambia:+“Na twende+ katika nyumba ya Yehova.”+   Miguu yetu ilisimama+Ndani ya malango yako, Ee Yerusalemu.+   Yerusalemu limejengwa kama jiji+Ambalo limeunganishwa pamoja kwa umoja,+   Ambalo makabila wamepanda kuelekea humo,+Makabila ya Yah,+Kama kikumbusho kwa Israeli+Ili kulishukuru jina la Yehova.+   Kwa maana huko viti vya ufalme vya hukumu vimewekwa,+Viti vya ufalme kwa ajili ya nyumba ya Daudi.+   Ombeni kwa ajili ya amani ya Yerusalemu.+Wanaokupenda, Ee jiji, hawatakuwa na wasiwasi.+   Amani na iendelee kuwa ndani ya boma lako,+Ukosefu wa wasiwasi ndani ya minara ya makao yako.+   Kwa ajili ya ndugu zangu na wenzangu nitasema sasa:+“Amani na iwe ndani yako.”+   Kwa ajili ya nyumba ya Yehova Mungu wetu+Nitaendelea kutafuta mema kwa ajili yako.+

Maelezo ya Chini