Zaburi 122:1-9
Wimbo wa Mipando. Wa Daudi.
122 Nilishangilia walipokuwa wakiniambia:+“Na twende+ katika nyumba ya Yehova.”+
2 Miguu yetu ilisimama+Ndani ya malango yako, Ee Yerusalemu.+
3 Yerusalemu limejengwa kama jiji+Ambalo limeunganishwa pamoja kwa umoja,+
4 Ambalo makabila wamepanda kuelekea humo,+Makabila ya Yah,+Kama kikumbusho kwa Israeli+Ili kulishukuru jina la Yehova.+
5 Kwa maana huko viti vya ufalme vya hukumu vimewekwa,+Viti vya ufalme kwa ajili ya nyumba ya Daudi.+
6 Ombeni kwa ajili ya amani ya Yerusalemu.+Wanaokupenda, Ee jiji, hawatakuwa na wasiwasi.+
7 Amani na iendelee kuwa ndani ya boma lako,+Ukosefu wa wasiwasi ndani ya minara ya makao yako.+
8 Kwa ajili ya ndugu zangu na wenzangu nitasema sasa:+“Amani na iwe ndani yako.”+
9 Kwa ajili ya nyumba ya Yehova Mungu wetu+Nitaendelea kutafuta mema kwa ajili yako.+