Zaburi 54:1-7

Kwa kiongozi wa vinanda. Maskili. Ya Daudi. Wakati Wazifu walipokuja na kumwambia Sauli: “Je, Daudi hajifichi pamoja nasi?”+ 54  Ee Mungu, uniokoe kwa jina lako,+Nawe unitetee katika kesi yangu kwa uwezo wako.+   Ee Mungu, uisikie sala yangu;+Utege sikio usikie maneno ya kinywa changu.+   Kwa maana kuna wageni ambao wameinuka dhidi yangu,Na waonevu wanaoitafuta nafsi yangu.+Hawajamweka Mungu mbele yao.+ Sela.   Tazama! Mungu ni msaidizi wangu;+Yehova yuko kati ya wale wanaoitegemeza nafsi yangu.   Atawalipa adui zangu ubaya;+Katika ukweli wako uwanyamazishe.+   Nitakutolea dhabihu kwa kupenda.+Nitalisifu jina lako, Ee Yehova, kwa maana ni jema.+   Kwa maana alinikomboa kutoka katika kila taabu,+Nalo jicho langu limewatazama adui zangu.+

Maelezo ya Chini