Zaburi 130:1-8
Wimbo wa Mipando.
130 Kutoka vilindini nimekuitia wewe, Ee Yehova.+
2 Ee Yehova, uisikie sauti yangu.+Masikio yako na yasikilize sauti ya kusihi kwangu.+
3 Kama ungekuwa unaangalia makosa,+ Ee Yah,Ee Yehova, ni nani angesimama?+
4 Kwa maana kwako wewe kuna msamaha wa kweli,+Ili upate kuogopwa.+
5 Nimetumainia, Ee Yehova, nafsi yangu imetumainia,+Nalo neno lake nimelingojea.+
6 Nafsi yangu imemngojea Yehova+Kuliko walinzi wanavyoingojea asubuhi,+Ambao wanaingojea asubuhi.+
7 Israeli na aendelee kumngojea Yehova.+Kwa maana kuna fadhili zenye upendo kwa Yehova,+Na ndivyo kulivyo na ukombozi mwingi kwake.+
8 Na yeye mwenyewe atamkomboa Israeli kutoka katika makosa yake yote.+