Zaburi 130:1-8

Wimbo wa Mipando. 130  Kutoka vilindini nimekuitia wewe, Ee Yehova.+   Ee Yehova, uisikie sauti yangu.+Masikio yako na yasikilize sauti ya kusihi kwangu.+   Kama ungekuwa unaangalia makosa,+ Ee Yah,Ee Yehova, ni nani angesimama?+   Kwa maana kwako wewe kuna msamaha wa kweli,+Ili upate kuogopwa.+   Nimetumainia, Ee Yehova, nafsi yangu imetumainia,+Nalo neno lake nimelingojea.+   Nafsi yangu imemngojea Yehova+Kuliko walinzi wanavyoingojea asubuhi,+Ambao wanaingojea asubuhi.+   Israeli na aendelee kumngojea Yehova.+Kwa maana kuna fadhili zenye upendo kwa Yehova,+Na ndivyo kulivyo na ukombozi mwingi kwake.+   Na yeye mwenyewe atamkomboa Israeli kutoka katika makosa yake yote.+

Maelezo ya Chini