Zaburi 3:1-8

Muziki wa Daudi alipokuwa akikimbia kwa sababu ya Absalomu mwana wake.+ 3  Ee Yehova, kwa nini adui zangu wamekuwa wengi?+Kwa nini wengi wanainuka dhidi yangu?+   Wengi wanasema juu ya nafsi yangu:“Hakuna wokovu kwa ajili yake kutoka kwa Mungu.”+ Sela.   Na bado wewe, Ee Yehova, ni ngao inayonizunguka,+Utukufu+ wangu na Mwenye kuinua kichwa changu.+   Kwa sauti yangu nitamwita Yehova,Naye atanijibu kutoka katika mlima wake mtakatifu.+ Sela.   Nami nitajilaza nipate kulala usingizi;Hakika nitaamka, kwa maana Yehova anaendelea kunitegemeza.+   Sitaogopa maelfu kumi ya watuAmbao wamejipanga dhidi yangu kunizunguka pande zote.+   Usimame,+ Ee Yehova! Uniokoe,+ Ee Mungu wangu!+Kwa maana utawapiga adui zangu wote kwenye taya.+Utayavunja meno ya waovu.+   Wokovu ni wa Yehova.+Baraka yako iko juu ya watu wako.+ Sela.

Maelezo ya Chini