Zaburi 3:1-8
Muziki wa Daudi alipokuwa akikimbia kwa sababu ya Absalomu mwana wake.+
3 Ee Yehova, kwa nini adui zangu wamekuwa wengi?+Kwa nini wengi wanainuka dhidi yangu?+
2 Wengi wanasema juu ya nafsi yangu:“Hakuna wokovu kwa ajili yake kutoka kwa Mungu.”+ Sela.
3 Na bado wewe, Ee Yehova, ni ngao inayonizunguka,+Utukufu+ wangu na Mwenye kuinua kichwa changu.+
4 Kwa sauti yangu nitamwita Yehova,Naye atanijibu kutoka katika mlima wake mtakatifu.+ Sela.
5 Nami nitajilaza nipate kulala usingizi;Hakika nitaamka, kwa maana Yehova anaendelea kunitegemeza.+
6 Sitaogopa maelfu kumi ya watuAmbao wamejipanga dhidi yangu kunizunguka pande zote.+
7 Usimame,+ Ee Yehova! Uniokoe,+ Ee Mungu wangu!+Kwa maana utawapiga adui zangu wote kwenye taya.+Utayavunja meno ya waovu.+
8 Wokovu ni wa Yehova.+Baraka yako iko juu ya watu wako.+ Sela.