Zaburi 124:1-8
Wimbo wa Mipando. Wa Daudi.
124 “Kama Yehova hangekuwa upande wetu,”+Sasa Israeli na aseme,+
2 “Kama Yehova hangekuwa upande wetu+Watu waliposimama dhidi yetu,+
3 Ndipo wangetumeza hata tukiwa hai,+Hasira yao ilipokuwa inawaka juu yetu.+
4 Ndipo maji yangetufagilia mbali,+Mto wenyewe ungepita juu ya nafsi yetu.+
5 Ndipo yangepita juu ya nafsi yetuMaji ya kimbelembele.+
6 Na abarikiwe Yehova, ambaye hakututoa+Tuwe mawindo kwa meno yao.+
7 Nafsi yetu ni kama ndege ambaye ameponyoka+Kutoka katika mtego wa watega-chambo.+Mtego umevunjwa,+Na sisi tumeponyoka.+
8 Msaada wetu uko katika jina la Yehova,+Mtengenezaji wa mbingu na dunia.”+