Zaburi 140:1-13
Kwa kiongozi. Muziki wa Daudi.
140 Uniokoe, Ee Yehova, kutoka kwa watu wabaya;+Unilinde na mtu mwenye matendo ya jeuri,+
2 Wale ambao wamepanga mambo mabaya moyoni mwao,+Ambao mchana kutwa wanaendelea kushambulia kama katika vita.+
3 Wameunoa ulimi wao kama ule wa nyoka;+Sumu ya kipiri-pembe iko chini ya midomo yao.+ Sela.
4 Unilinde, Ee Yehova, na mikono ya mwovu;+Unilinde na mtu mwenye matendo ya jeuri,+Wale ambao wamepanga hila ya kuzisukuma hatua zangu.+
5 Waliojiinua wenyewe wameficha mtego kwa ajili yangu;+Nao wamezitandika kamba kama wavu kando ya njia.+Wametega minaso kwa ajili yangu.+ Sela.
6 Nimemwambia Yehova: “Wewe ni Mungu wangu.+Utege sikio, Ee Yehova, usikie sauti ya kusihi kwangu.”+
7 Ee Yehova Bwana Mwenye Enzi Kuu,+ nguvu za wokovu wangu,+Umekinga kichwa changu katika siku ya jeshi lenye silaha.+
8 Ee Yehova, usimpe mwovu tamaa zake.+Usiunge mkono hila yake, ili wasipate kuinuliwa.+ Sela.
9 Navyo vichwa vya wale wanaonizunguka,+Taabu ya midomo yao wenyewe na ivifunike.+
10 Makaa yanayowaka moto na yaangushwe juu yao.+Na waangushwe motoni,+ ndani ya mashimo yenye maji, ili wasipate kusimama.+
11 Yule mwenye kuongea makuu—na asifanywe imara duniani.+Mtu wa jeuri—uovu na umwinde kwa mapigo yenye kurudiwa.+
12 Najua vema kwamba Yehova atatimiza+Dai halali la mwenye kuteseka, hukumu ya maskini.+
13 Hakika waadilifu watalishukuru jina lako;+Wanyoofu watakaa mbele za uso wako.+