Zaburi 126:1-6
Wimbo wa Mipando.
126 Yehova alipowakusanya tena mateka wa Sayuni,+Tulikuwa kama wale waliokuwa wanaota ndoto.+
2 Wakati huo kinywa chetu kilijaa kicheko,+Na ulimi wetu vigelegele vya shangwe.+Wakati huo walianza kusema kati ya mataifa:+“Yehova amefanya jambo kuu katika yale ambayo amewafanyia.”+
3 Yehova amefanya jambo kuu katika yale ambayo ametufanyia.+Tumekuwa na shangwe.+
4 Ee Yehova, uirudishe jamii yetu ya mateka,+Kama sakafu za vijito katika Negebu.+
5 Wale wanaopanda mbegu kwa machozi+Watavuna kwa vigelegele vya shangwe.+
6 Yule ambaye bila shaka anaenda, naam, akilia,+Akiwa amechukua mfuko uliojaa mbegu,+Bila shaka ataingia kwa vigelegele vya shangwe,+Akiwa amechukua miganda yake.+