Zaburi 126:1-6

Wimbo wa Mipando. 126  Yehova alipowakusanya tena mateka wa Sayuni,+Tulikuwa kama wale waliokuwa wanaota ndoto.+   Wakati huo kinywa chetu kilijaa kicheko,+Na ulimi wetu vigelegele vya shangwe.+Wakati huo walianza kusema kati ya mataifa:+“Yehova amefanya jambo kuu katika yale ambayo amewafanyia.”+   Yehova amefanya jambo kuu katika yale ambayo ametufanyia.+Tumekuwa na shangwe.+   Ee Yehova, uirudishe jamii yetu ya mateka,+Kama sakafu za vijito katika Negebu.+   Wale wanaopanda mbegu kwa machozi+Watavuna kwa vigelegele vya shangwe.+   Yule ambaye bila shaka anaenda, naam, akilia,+Akiwa amechukua mfuko uliojaa mbegu,+Bila shaka ataingia kwa vigelegele vya shangwe,+Akiwa amechukua miganda yake.+

Maelezo ya Chini