Zaburi 5:1-12
Kwa kiongozi wa Nehilothi. Muziki wa Daudi.
5 Kwa maneno yangu utege sikio,+ Ee Yehova;Uelewe kuugua kwangu.
2 Sikiliza kwa makini sauti ya kilio changu kwa ajili ya msaada,+Ee Mfalme+ wangu na Mungu wangu, kwa maana kwako wewe ninasali.+
3 Ee Yehova, asubuhi utasikia sauti yangu;+Asubuhi nitajieleza kwako na kukaa macho.+
4 Kwa maana wewe si Mungu anayependezwa na uovu;+Hakuna mtu yeyote mbaya atakayekaa na wewe kwa muda wowote.+
5 Hakuna watu wowote wenye kujisifu watakaosimama mbele za macho yako.+Wewe huwachukia wote wanaozoea kufanya mambo yenye kuumiza;+
6 Utawaangamiza wale wanaosema uwongo.+Mtu anayemwaga damu+ na mdanganyifu+ Yehova anamchukia.
7 Na mimi, katika wingi wa fadhili zako zenye upendo+Nitaingia katika nyumba yako,+Nitainama kulielekea hekalu lako takatifu kwa kukuogopa.+
8 Ee Yehova, uniongoze katika uadilifu+ wako kwa sababu ya adui zangu;+Uifanye njia yako iwe laini mbele yangu.+
9 Kwa maana katika kinywa chao hakuna lolote lenye kutegemeka;+Sehemu yao ya ndani ni shida kwelikweli.+Koo yao ni kaburi lililo wazi;+Wanatumia ulimi laini.+
10 Hakika Mungu atawahesabia hatia;+Wataanguka kwa sababu ya mashauri yao wenyewe.+Na watawanywe katika wingi wa makosa yao,+Kwa sababu wamekuasi wewe.+
11 Lakini wote wanaokukimbilia watashangilia;+Watapiga vigelegele vya shangwe+ mpaka wakati usio na kipimo.Nawe utaweka kizuizi wasifikiwe,Nao wanaolipenda jina lako watakushangilia.+
12 Kwa maana wewe mwenyewe utambariki mtu yeyote aliye mwadilifu,+ Ee Yehova;Kana kwamba kwa ngao+ kubwa, utawazunguka pande zote+ kwa kibali chako.