Zaburi 5:1-12

Kwa kiongozi wa Nehilothi. Muziki wa Daudi. 5  Kwa maneno yangu utege sikio,+ Ee Yehova;Uelewe kuugua kwangu.   Sikiliza kwa makini sauti ya kilio changu kwa ajili ya msaada,+Ee Mfalme+ wangu na Mungu wangu, kwa maana kwako wewe ninasali.+   Ee Yehova, asubuhi utasikia sauti yangu;+Asubuhi nitajieleza kwako na kukaa macho.+   Kwa maana wewe si Mungu anayependezwa na uovu;+Hakuna mtu yeyote mbaya atakayekaa na wewe kwa muda wowote.+   Hakuna watu wowote wenye kujisifu watakaosimama mbele za macho yako.+Wewe huwachukia wote wanaozoea kufanya mambo yenye kuumiza;+   Utawaangamiza wale wanaosema uwongo.+Mtu anayemwaga damu+ na mdanganyifu+ Yehova anamchukia.   Na mimi, katika wingi wa fadhili zako zenye upendo+Nitaingia katika nyumba yako,+Nitainama kulielekea hekalu lako takatifu kwa kukuogopa.+   Ee Yehova, uniongoze katika uadilifu+ wako kwa sababu ya adui zangu;+Uifanye njia yako iwe laini mbele yangu.+   Kwa maana katika kinywa chao hakuna lolote lenye kutegemeka;+Sehemu yao ya ndani ni shida kwelikweli.+Koo yao ni kaburi lililo wazi;+Wanatumia ulimi laini.+ 10  Hakika Mungu atawahesabia hatia;+Wataanguka kwa sababu ya mashauri yao wenyewe.+Na watawanywe katika wingi wa makosa yao,+Kwa sababu wamekuasi wewe.+ 11  Lakini wote wanaokukimbilia watashangilia;+Watapiga vigelegele vya shangwe+ mpaka wakati usio na kipimo.Nawe utaweka kizuizi wasifikiwe,Nao wanaolipenda jina lako watakushangilia.+ 12  Kwa maana wewe mwenyewe utambariki mtu yeyote aliye mwadilifu,+ Ee Yehova;Kana kwamba kwa ngao+ kubwa, utawazunguka pande zote+ kwa kibali chako.

Maelezo ya Chini