Zaburi 10:1-18
ל [Laʹmedh]
10 Ee Yehova, kwa nini unaendelea kusimama mbali?+Kwa nini unaendelea kujificha nyakati za taabu?+
2 Katika majivuno yake, mwovu humfuatilia vikali mwenye kuteseka;+Wanakamatwa na mawazo ambayo wametunga.+
3 Kwa maana mwovu amejisifu kwa sababu ya tamaa yenye ubinafsi ya nafsi yake,+Naye anayepata faida asiyostahili+ amejibariki;נ [Nun]Amekosa kumheshimu Yehova.+
4 Kwa sababu ya kujigamba kwake, mwovu hatafuti;+Mawazo yake yote ni: “Hakuna Mungu.”+
5 Njia zake zinaendelea kufanikiwa wakati wote.+Maamuzi yako ya hukumu yako juu sana asiweze kuyafikia;+Nao wale wote wanaomwonyesha uadui, anawafanyia dhihaka.+
6 Amesema katika moyo wake: “Sitatikiswa;+Kizazi baada ya kizazi sitakuwa katika msiba.”+
פ [Peʼ]
7 Kinywa chake kimejaa viapo na udanganyifu na ukandamizaji.+Chini ya ulimi wake kuna taabu na mambo yenye kuumiza.+
8 Yeye huketi akivizia makao;Kutoka mafichoni atamuua mtu asiye na hatia.+
ע [ʽAʹyin]Macho yake yanamtafuta mtu mwenye taabu.+
9 Yeye anaendelea kuvizia katika mahali palipofichika kama simba mafichoni mwake.+Anaendelea kuvizia+ ili amchukue kwa nguvu mtu fulani mwenye kuteseka.Humchukua kwa nguvu mtu mwenye kuteseka anapouvuta pamoja wavu wake.+
10 Yeye anapondwa, anainama,Na jeshi la watu waliohuzunika linaangukia kucha zake zenye nguvu.+
11 Yeye amesema katika moyo wake:+ “Mungu amesahau.+Ameuficha uso wake.+Hakika hatauona kamwe.”+
ק [Qohph]
12 Usimame,+ Ee Yehova. Ee Mungu, uinue mkono wako.+Usiwasahau wenye kuteseka.+
13 Kwa nini mwovu amekosa kumheshimu Mungu?+Amesema katika moyo wake: “Wewe hutatoza hesabu.”+
ר [Rehsh]
14 Kwa maana wewe mwenyewe umeona taabu na masumbufu.Unaendelea kutazama, uyatie katika mkono wako.+Mtu mwenye taabu,+ mvulana asiye na baba, anajikabidhi kwako.Wewe mwenyewe umekuwa msaidizi wake.+
ש [Shin]
15 Uvunje mkono wa mwovu na mbaya.+Uutafute uovu wake mpaka usiupate tena.+
16 Yehova ni Mfalme mpaka wakati usio na kipimo, naam, milele.+Mataifa yameangamia kutoka katika dunia yake.+
ת [Taw]
17 Tamaa ya wapole hakika utaisikia,+ Ee Yehova.Utautayarisha moyo wao.+Utasikiliza kwa makini kwa sikio lako.+
18 Ili kumhukumu mvulana asiye na baba na mtu aliyepondwa,+Ili mwanadamu anayeweza kufa, aliye wa dunia, asisababishe tena kutetemeka.+