Zaburi 10:1-18

ל [Laʹmedh] 10  Ee Yehova, kwa nini unaendelea kusimama mbali?+Kwa nini unaendelea kujificha nyakati za taabu?+   Katika majivuno yake, mwovu humfuatilia vikali mwenye kuteseka;+Wanakamatwa na mawazo ambayo wametunga.+   Kwa maana mwovu amejisifu kwa sababu ya tamaa yenye ubinafsi ya nafsi yake,+Naye anayepata faida asiyostahili+ amejibariki;נ [Nun]Amekosa kumheshimu Yehova.+   Kwa sababu ya kujigamba kwake, mwovu hatafuti;+Mawazo yake yote ni: “Hakuna Mungu.”+   Njia zake zinaendelea kufanikiwa wakati wote.+Maamuzi yako ya hukumu yako juu sana asiweze kuyafikia;+Nao wale wote wanaomwonyesha uadui, anawafanyia dhihaka.+   Amesema katika moyo wake: “Sitatikiswa;+Kizazi baada ya kizazi sitakuwa katika msiba.”+ פ [Peʼ]   Kinywa chake kimejaa viapo na udanganyifu na ukandamizaji.+Chini ya ulimi wake kuna taabu na mambo yenye kuumiza.+   Yeye huketi akivizia makao;Kutoka mafichoni atamuua mtu asiye na hatia.+ ע [ʽAʹyin]Macho yake yanamtafuta mtu mwenye taabu.+   Yeye anaendelea kuvizia katika mahali palipofichika kama simba mafichoni mwake.+Anaendelea kuvizia+ ili amchukue kwa nguvu mtu fulani mwenye kuteseka.Humchukua kwa nguvu mtu mwenye kuteseka anapouvuta pamoja wavu wake.+ 10  Yeye anapondwa, anainama,Na jeshi la watu waliohuzunika linaangukia kucha zake zenye nguvu.+ 11  Yeye amesema katika moyo wake:+ “Mungu amesahau.+Ameuficha uso wake.+Hakika hatauona kamwe.”+ ק [Qohph] 12  Usimame,+ Ee Yehova. Ee Mungu, uinue mkono wako.+Usiwasahau wenye kuteseka.+ 13  Kwa nini mwovu amekosa kumheshimu Mungu?+Amesema katika moyo wake: “Wewe hutatoza hesabu.”+ ר [Rehsh] 14  Kwa maana wewe mwenyewe umeona taabu na masumbufu.Unaendelea kutazama, uyatie katika mkono wako.+Mtu mwenye taabu,+ mvulana asiye na baba, anajikabidhi kwako.Wewe mwenyewe umekuwa msaidizi wake.+ ש [Shin] 15  Uvunje mkono wa mwovu na mbaya.+Uutafute uovu wake mpaka usiupate tena.+ 16  Yehova ni Mfalme mpaka wakati usio na kipimo, naam, milele.+Mataifa yameangamia kutoka katika dunia yake.+ ת [Taw] 17  Tamaa ya wapole hakika utaisikia,+ Ee Yehova.Utautayarisha moyo wao.+Utasikiliza kwa makini kwa sikio lako.+ 18  Ili kumhukumu mvulana asiye na baba na mtu aliyepondwa,+Ili mwanadamu anayeweza kufa, aliye wa dunia, asisababishe tena kutetemeka.+

Maelezo ya Chini