Zaburi 73:1-28
Muziki wa Asafu.+
73 Kwa kweli Mungu ni mwema kwa Israeli, kwa wale walio safi moyoni.+
2 Mimi nami karibu miguu yangu igeuke kando,+Hatua zangu zilikuwa karibu kuteleza.+
3 Kwa maana niliwaonea wivu wenye kujisifu,+Nilipokuwa nikiiona amani ya watu waovu.+
4 Kwa maana hawana maumivu ya kifo;+Na kitambi chao ni kinono.+
5 Wala hawamo katika taabu ya mwanadamu anayeweza kufa,+Wala hawapati mapigo kama wanadamu wengine.+
6 Kwa hiyo majivuno yamekuwa mkufu shingoni pao;+Jeuri huwafunika kama vazi.+
7 Jicho lao limevimba kwa sababu ya unono;+Wamezidi mawazo ya moyo.+
8 Wao hudhihaki na kuzungumza juu ya yaliyo mabaya;+Wanazungumza juu ya upunjaji kwa majivuno.+
9 Wameweka kinywa chao mbinguni,+Nao ulimi wao hutembea huku na huku duniani.+
10 Kwa hiyo yeye huwarudisha watu wake hapa,Na maji yaliyojaa yanakaushwa kwa ajili yao.
11 Nao wamesema: “Mungu amepataje kujua?+Na je, Aliye Juu Zaidi ana ujuzi?”+
12 Tazama! Hao ndio waovu waliostarehe mpaka wakati usio na kipimo.+Wameongeza mali yao.+
13 Hakika nimeusafisha moyo wangu bure+Na kuiosha mikono yangu katika kutokuwa na hatia.+
14 Nami nikapata mapigo mchana kutwa,+Na rekebisho langu ni la kila asubuhi.+
15 Kama ningelisema: “Nitasimulia hadithi kama hiyo,”Tazama! juu ya kizazi cha wana wakoNingelitenda kwa hila.+
16 Nami nikaendelea kufikiria ili nijue hilo;+Lilikuwa ni taabu machoni pangu.
17 Mpaka nilipoingia katika patakatifu pakuu pa Mungu.+Nilitaka kuutambua wakati wao ujao.+
18 Hakika unawaweka kwenye udongo unaoteleza.+Umewafanya waanguke kwenye uharibifu.+
19 Lo! Jinsi wamekuwa kitu cha kushangaza ghafula!+Jinsi wameufikia mwisho wao, wamemalizwa kwa matisho ya ghafula!
20 Kama ndoto baada ya kuamka, Ee Yehova,+Ndivyo utakavyoidharau sura yao utakapoamka.+
21 Kwa maana moyo wangu ulikuwa umetiwa uchungu+Nami nilikuwa na maumivu makali kwenye figo zangu.+
22 Nami sikutumia akili wala singeweza kujua;+Nilikuwa kama wanyama tu kwa maoni yako.+
23 Lakini niko pamoja nawe daima;+Umeushika mkono wangu wa kuume.+
24 Utaniongoza kwa shauri lako,+Na baadaye utanipeleka kwenye utukufu.+
25 Ni nani niliye naye mbinguni?+Na isipokuwa wewe sina mapendezi mengine duniani.+
26 Mwili wangu na moyo wangu vimeshindwa.+Mungu ni mwamba wa moyo wangu na fungu langu mpaka wakati usio na kipimo.+
27 Kwa maana, tazama! Walewale wanaokaa mbali nawe wataangamia.+Hakika utamnyamazisha kila mtu ambaye kwa njia isiyo ya adili anakuacha.+
28 Lakini mimi, kumkaribia Mungu ni kwema kwangu.+Nimeweka kimbilio langu katika Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova,+Ili kutangaza kazi zako zote.+