Zaburi 73:1-28

Muziki wa Asafu.+ 73  Kwa kweli Mungu ni mwema kwa Israeli, kwa wale walio safi moyoni.+   Mimi nami karibu miguu yangu igeuke kando,+Hatua zangu zilikuwa karibu kuteleza.+   Kwa maana niliwaonea wivu wenye kujisifu,+Nilipokuwa nikiiona amani ya watu waovu.+   Kwa maana hawana maumivu ya kifo;+Na kitambi chao ni kinono.+   Wala hawamo katika taabu ya mwanadamu anayeweza kufa,+Wala hawapati mapigo kama wanadamu wengine.+   Kwa hiyo majivuno yamekuwa mkufu shingoni pao;+Jeuri huwafunika kama vazi.+   Jicho lao limevimba kwa sababu ya unono;+Wamezidi mawazo ya moyo.+   Wao hudhihaki na kuzungumza juu ya yaliyo mabaya;+Wanazungumza juu ya upunjaji kwa majivuno.+   Wameweka kinywa chao mbinguni,+Nao ulimi wao hutembea huku na huku duniani.+ 10  Kwa hiyo yeye huwarudisha watu wake hapa,Na maji yaliyojaa yanakaushwa kwa ajili yao. 11  Nao wamesema: “Mungu amepataje kujua?+Na je, Aliye Juu Zaidi ana ujuzi?”+ 12  Tazama! Hao ndio waovu waliostarehe mpaka wakati usio na kipimo.+Wameongeza mali yao.+ 13  Hakika nimeusafisha moyo wangu bure+Na kuiosha mikono yangu katika kutokuwa na hatia.+ 14  Nami nikapata mapigo mchana kutwa,+Na rekebisho langu ni la kila asubuhi.+ 15  Kama ningelisema: “Nitasimulia hadithi kama hiyo,”Tazama! juu ya kizazi cha wana wakoNingelitenda kwa hila.+ 16  Nami nikaendelea kufikiria ili nijue hilo;+Lilikuwa ni taabu machoni pangu. 17  Mpaka nilipoingia katika patakatifu pakuu pa Mungu.+Nilitaka kuutambua wakati wao ujao.+ 18  Hakika unawaweka kwenye udongo unaoteleza.+Umewafanya waanguke kwenye uharibifu.+ 19  Lo! Jinsi wamekuwa kitu cha kushangaza ghafula!+Jinsi wameufikia mwisho wao, wamemalizwa kwa matisho ya ghafula! 20  Kama ndoto baada ya kuamka, Ee Yehova,+Ndivyo utakavyoidharau sura yao utakapoamka.+ 21  Kwa maana moyo wangu ulikuwa umetiwa uchungu+Nami nilikuwa na maumivu makali kwenye figo zangu.+ 22  Nami sikutumia akili wala singeweza kujua;+Nilikuwa kama wanyama tu kwa maoni yako.+ 23  Lakini niko pamoja nawe daima;+Umeushika mkono wangu wa kuume.+ 24  Utaniongoza kwa shauri lako,+Na baadaye utanipeleka kwenye utukufu.+ 25  Ni nani niliye naye mbinguni?+Na isipokuwa wewe sina mapendezi mengine duniani.+ 26  Mwili wangu na moyo wangu vimeshindwa.+Mungu ni mwamba wa moyo wangu na fungu langu mpaka wakati usio na kipimo.+ 27  Kwa maana, tazama! Walewale wanaokaa mbali nawe wataangamia.+Hakika utamnyamazisha kila mtu ambaye kwa njia isiyo ya adili anakuacha.+ 28  Lakini mimi, kumkaribia Mungu ni kwema kwangu.+Nimeweka kimbilio langu katika Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova,+Ili kutangaza kazi zako zote.+

Maelezo ya Chini