Zaburi 32:1-11
Ya Daudi. Maskili.
32 Mwenye furaha ni mtu ambaye amesamehewa maasi yake, ambaye dhambi yake imefunikwa.+
2 Mwenye furaha ni mtu ambaye Yehova hamhesabii kosa,+Na ambaye katika roho yake hamna udanganyifu.+
3 Nilipokaa kimya mifupa yangu ilichakaa kwa sababu ya kuugua kwangu mchana kutwa.+
4 Kwa maana mkono wako ulikuwa mzito juu yangu mchana na usiku.+Umajimaji wa uhai wangu umenyauka kama wakati wa joto kavu la kiangazi.+ Sela.
5 Mwishowe niliungama dhambi yangu kwako, wala sikufunika kosa langu.+Nilisema: “Nitaungama makosa yangu kwa Yehova.”+Nawe mwenyewe ukanisamehe kosa la dhambi zangu.+ Sela.
6 Kwa sababu hiyo kila aliye mshikamanifu atasali kwako+Katika wakati ule tu ambao wewe unaweza kupatikana.+Nayo mafuriko ya maji mengi hayatamgusa.+
7 Wewe ni mahali pangu pa kujificha; utanilinda kutokana na taabu.+Utanizingira kwa vigelegele vya shangwe kwa sababu ya kuniokoa.+ Sela.
8 “Nitakufanya uwe na ufahamu na kukufundisha katika njia unayopaswa kuiendea.+Nitakupa shauri jicho langu likiwa linakutazama.+
9 Msijifanye kama farasi au nyumbu wasio na uelewaji,+Ambao roho yao yenye nguvu huzuiwa na hatamu au lijamu+Kabla wao hawajakukaribia wewe.”+
10 Mwovu ana maumivu mengi;+Lakini mtu anayemtegemea Yehova, fadhili zenye upendo humzingira.+
11 Shangilieni katika Yehova na kuwa na shangwe, enyi waadilifu;+Na mpige vigelegele vya shangwe, ninyi nyote mlio wanyoofu katika moyo.+