Zaburi 143:1-12
Muziki wa Daudi.
143 Ee Yehova, uisikie sala yangu;+Utege sikio usikie kusihi kwangu.+Katika uaminifu wako unijibu kwa uadilifu wako.+
2 Wala usiingie katika hukumu pamoja na mtumishi wako;+Kwa maana mbele zako, hakuna yeyote aliye hai anayeweza kuwa mwadilifu.+
3 Kwa maana adui ameifuatilia nafsi yangu;+Ameuponda uhai wangu mpaka chini.+Amenifanya nikae katika mahali penye giza kama wale waliokufa kwa wakati usio na kipimo.+
4 Na roho+ yangu inazimia ndani yangu;Moyo wangu wenyewe umekufa ganzi katikati yangu.+
5 Nimezikumbuka siku za zamani za kale;+Nimetafakari juu ya utendaji wako wote;+Kwa kupenda niliendelea kuhangaikia kazi ya mikono yako mwenyewe.+
6 Nimekunyooshea mikono yangu;+Nafsi yangu kwako ni kama nchi iliyochoka kabisa.+ Sela.
7 Ufanye haraka, unijibu, Ee Yehova.+Roho yangu imefikia mwisho.+Usiufiche uso wako mbali nami,+Kama sivyo nitakuwa kama wale wanaoshuka kuingia shimoni.+
8 Asubuhi unifanye nisikie fadhili zako zenye upendo,+Kwa maana nimekutegemea wewe.+Unijulishe njia ninayopaswa kuitembea,+Kwa maana nimekuinulia nafsi yangu.+
9 Unikomboe kutoka kwa adui zangu, Ee Yehova.+Nimejificha kwako.+
10 Unifundishe kufanya mapenzi yako,+Kwa maana wewe ni Mungu wangu.+Roho yako ni nzuri;+Na iniongoze katika nchi ya unyoofu.+
11 Kwa ajili ya jina lako,+ Ee Yehova, unihifadhi hai.+Katika uadilifu+ wako na uitoe nafsi yangu katika taabu.+
12 Na katika fadhili zako zenye upendo uwanyamazishe adui zangu;+Nawe uwaangamize wote wanaoichukia nafsi yangu,+Kwa maana mimi ni mtumishi wako.+