Zaburi 143:1-12

Muziki wa Daudi. 143  Ee Yehova, uisikie sala yangu;+Utege sikio usikie kusihi kwangu.+Katika uaminifu wako unijibu kwa uadilifu wako.+   Wala usiingie katika hukumu pamoja na mtumishi wako;+Kwa maana mbele zako, hakuna yeyote aliye hai anayeweza kuwa mwadilifu.+   Kwa maana adui ameifuatilia nafsi yangu;+Ameuponda uhai wangu mpaka chini.+Amenifanya nikae katika mahali penye giza kama wale waliokufa kwa wakati usio na kipimo.+   Na roho+ yangu inazimia ndani yangu;Moyo wangu wenyewe umekufa ganzi katikati yangu.+   Nimezikumbuka siku za zamani za kale;+Nimetafakari juu ya utendaji wako wote;+Kwa kupenda niliendelea kuhangaikia kazi ya mikono yako mwenyewe.+   Nimekunyooshea mikono yangu;+Nafsi yangu kwako ni kama nchi iliyochoka kabisa.+ Sela.   Ufanye haraka, unijibu, Ee Yehova.+Roho yangu imefikia mwisho.+Usiufiche uso wako mbali nami,+Kama sivyo nitakuwa kama wale wanaoshuka kuingia shimoni.+   Asubuhi unifanye nisikie fadhili zako zenye upendo,+Kwa maana nimekutegemea wewe.+Unijulishe njia ninayopaswa kuitembea,+Kwa maana nimekuinulia nafsi yangu.+   Unikomboe kutoka kwa adui zangu, Ee Yehova.+Nimejificha kwako.+ 10  Unifundishe kufanya mapenzi yako,+Kwa maana wewe ni Mungu wangu.+Roho yako ni nzuri;+Na iniongoze katika nchi ya unyoofu.+ 11  Kwa ajili ya jina lako,+ Ee Yehova, unihifadhi hai.+Katika uadilifu+ wako na uitoe nafsi yangu katika taabu.+ 12  Na katika fadhili zako zenye upendo uwanyamazishe adui zangu;+Nawe uwaangamize wote wanaoichukia nafsi yangu,+Kwa maana mimi ni mtumishi wako.+

Maelezo ya Chini