Zaburi 20:1-9
Kwa kiongozi. Muziki wa Daudi.
20 Yehova na akujibu siku ya taabu.+Jina la Mungu wa Yakobo na likulinde.+
2 Na atume msaada wako kutoka katika mahali patakatifu,+Na kukutegemeza kutoka Sayuni.+
3 Na akumbuke matoleo yako yote ya zawadi,+Naye na ayakubali matoleo yako ya kuteketezwa kuwa ni mafuta.+ Sela.
4 Na akupe kulingana na moyo wako,+Naye na alitimize kusudi lako lote.+
5 Tutapiga vigelegele kwa shangwe kwa sababu ya wokovu wako,+Nasi tutainua bendera zetu katika jina la Mungu wetu.+Yehova na atimize maombi yako yote.+
6 Sasa najua kwamba hakika Yehova humwokoa mtiwa-mafuta wake.+Humjibu kutoka katika mbingu zake takatifu+
Kwa matendo ya kuokoa yenye nguvu ya mkono wake wa kuume.+
7 Wengine hutaja kuhusu magari na wengine kuhusu farasi,+Lakini sisi, tutataja kuhusu jina la Yehova Mungu wetu.+
8 Hao wamevunjika na kuanguka;+Lakini sisi, tumesimama, ili tupate kurudishwa.+
9 Ee Yehova, umwokoe mfalme!+Yeye atatujibu siku ambayo tutaita.+