Zaburi 20:1-9

Kwa kiongozi. Muziki wa Daudi. 20  Yehova na akujibu siku ya taabu.+Jina la Mungu wa Yakobo na likulinde.+   Na atume msaada wako kutoka katika mahali patakatifu,+Na kukutegemeza kutoka Sayuni.+   Na akumbuke matoleo yako yote ya zawadi,+Naye na ayakubali matoleo yako ya kuteketezwa kuwa ni mafuta.+ Sela.   Na akupe kulingana na moyo wako,+Naye na alitimize kusudi lako lote.+   Tutapiga vigelegele kwa shangwe kwa sababu ya wokovu wako,+Nasi tutainua bendera zetu katika jina la Mungu wetu.+Yehova na atimize maombi yako yote.+   Sasa najua kwamba hakika Yehova humwokoa mtiwa-mafuta wake.+Humjibu kutoka katika mbingu zake takatifu+ Kwa matendo ya kuokoa yenye nguvu ya mkono wake wa kuume.+   Wengine hutaja kuhusu magari na wengine kuhusu farasi,+Lakini sisi, tutataja kuhusu jina la Yehova Mungu wetu.+   Hao wamevunjika na kuanguka;+Lakini sisi, tumesimama, ili tupate kurudishwa.+   Ee Yehova, umwokoe mfalme!+Yeye atatujibu siku ambayo tutaita.+

Maelezo ya Chini