Zaburi 47:1-9
Kwa kiongozi. Ya wana wa Kora. Muziki.
47 Enyi vikundi vyote vya watu, pigeni makofi.+Mpigieni Mungu kelele za ushindi kwa vigelegele vya shangwe.+
2 Kwa maana Yehova, Aliye Juu Zaidi, ni mwenye kuogopesha,+Mfalme mkuu juu ya dunia yote.+
3 Atatiisha vikundi vya watu chini yetu+Na vikundi vya mataifa chini ya miguu yetu.+
4 Atatuchagulia urithi wetu,+Fahari ya Yakobo, ambaye amempenda.+ Sela.
5 Mungu amepanda juu kwa vigelegele vya shangwe,+Yehova kwa sauti ya baragumu.+
6 Mpigieni Mungu muziki, pigeni muziki.+Mpigieni Mfalme wetu muziki, pigeni muziki.
7 Kwa maana Mungu ni Mfalme wa dunia yote;+Pigeni muziki, mkitenda kwa busara.+
8 Mungu amekuwa mfalme juu ya mataifa.+Mungu mwenyewe ameketi juu ya kiti chake kitakatifu cha ufalme.+
9 Wakuu wa watu wamekusanyika pamoja,+Pamoja na watu wa Mungu wa Abrahamu.+Kwa maana ngao za dunia ni za Mungu.+Yeye amepanda juu sana.+