Zaburi 79:1-13
Muziki wa Asafu.
79 Ee Mungu, mataifa yameingia katika urithi wako;+Wamelitia unajisi hekalu lako takatifu;+Wamefanya Yerusalemu kuwa rundo la mabomoko.+
2 Wamewapa ndege wa mbinguni maiti ya watumishi wako iwe chakula chao,+Na nyama ya washikamanifu wako kwa wanyama-mwitu wa dunia.+
3 Wamemwaga damu yao kama majiKuzunguka Yerusalemu pande zote, wala hakuna mtu wa kuzika.+
4 Tumekuwa shutuma kwa jirani zetu,+Dharau na dhihaka kwa wale wanaotuzunguka pande zote.+
5 Ee Yehova, utapandwa na hasira mpaka wakati gani? Milele?+Hasira yako itawaka kama moto mpaka wakati gani?+
6 Mwaga ghadhabu yako juu ya mataifa ambayo hayakukujua,+Na juu ya falme ambazo hazikuliitia jina lako.+
7 Kwa maana wamemla Yakobo,+Nao wamefanya makao yake yawe ukiwa.+
8 Usikumbuke dhidi yetu makosa ya mababu zetu.+Ufanye haraka! Rehema zako na zitufikie,+Kwa maana tumekuwa maskini sana.+
9 Utusaidie, Ee Mungu wa wokovu wetu,+Kwa ajili ya utukufu wa jina lako;+Na utukomboe na kufunika dhambi zetu kwa sababu ya jina lako.+
10 Kwa nini mataifa yaseme: “Mungu wao yuko wapi?”+Na ijulikane katika mataifa mbele ya macho yetu+Juu ya kulipiza kisasi damu ya watumishi wako ambayo imemwagwa.+
11 Kuugua kwa mfungwa na kuingie mbele zako.+Kulingana na ukuu wa mkono wako, uwahifadhi wale waliochaguliwa kwa ajili ya kifo.+
12 Na kuwalipa jirani zetu mara saba kifuani mwao+Shutuma yao ambayo wamekushutumu nayo, Ee Yehova.+
13 Na sisi watu wako na kundi la malisho yako,+Tutakushukuru mpaka wakati usio na kipimo;Kutoka kizazi mpaka kizazi tutatangaza sifa yako.+