Zaburi 78:1-72

Maskili. Ya Asafu.+ 78  Sikilizeni sheria yangu, enyi watu wangu;+Tegeni sikio lenu kwa maneno ya kinywa changu.+   Katika neno la kimethali nitakifungua kinywa changu;+Nitafanya vitendawili vya zamani za kale vibubujike,+   Ambavyo tumevisikia na tunavijua,+Na ambavyo baba zetu wenyewe wametusimulia;+   Ambavyo hatuwafichi wana wao,+Tukivisimulia hata kwa kizazi kitakachokuja,+Sifa za Yehova na nguvu zake+Na mambo yake ya ajabu ambayo amefanya.+   Naye akatokeza kikumbusho katika Yakobo,+Na sheria akaiweka katika Israeli,+Mambo ambayo aliwaamuru mababu zetu,+Wawajulishe wana wao;+   Ili kizazi kitakachokuja, wana ambao wangezaliwa, wapate kuyajua,+Ili wasimame na kuwasimulia wana wao,+   Na kwamba wao watie uhakika wao katika Mungu+Nao wasisahau matendo ya Mungu+ bali washike amri zake.+   Nao wasiwe kama mababu zao,+Kizazi chenye ukaidi na chenye kuasi,+Kizazi ambacho hakikuwa kimetayarisha moyo wake+Na ambacho roho yake haikuwa yenye kutegemeka kwa Mungu.+   Wana wa Efraimu, wajapokuwa ni wapiga-upinde wenye silaha,+Walirudi nyuma siku ya pigano.+ 10  Hawakulishika agano la Mungu,+Nao wakakataa kutembea katika sheria yake.+ 11  Pia wakaanza kusahau matendo yake+Na kazi zake za ajabu alizowafanya waone.+ 12  Mbele ya mababu zao yeye alikuwa ametenda kwa njia ya ajabu.+Katika nchi ya Misri,+ kiwanja cha Soani.+ 13  Aliipasua bahari, ili awaruhusu kuvuka,+Naye akayafanya maji yasimame kama bwawa.+ 14  Naye akaendelea kuwaongoza kwa wingu wakati wa mchana+Na usiku kucha kwa nuru ya moto.+ 15  Aliipasua miamba nyikani,+Ili awanyweshe kwa wingi kama vilindi vya maji.+ 16  Naye akatokeza vijito katika mwamba+Na kufanya maji yateremke kama mito.+ 17  Nao wakaendelea kumtendea dhambi hata zaidi+Kwa kumwasi Aliye Juu Zaidi katika eneo lisilo na maji;+ 18  Nao wakamjaribu Mungu moyoni mwao+Kwa kuomba chakula kwa ajili ya nafsi yao.+ 19  Basi wakaanza kusema vibaya juu ya Mungu.+Walisema: “Je, Mungu anaweza kutayarisha meza nyikani?”+ 20  Tazama! Alipiga mwamba+Ili maji yatiririke na mito ifurike.+“Je, anaweza pia kutoa mkate,+Au je, anaweza kuwatayarishia watu wake chakula?”+ 21  Ndiyo sababu Yehova alisikia, akaanza kuwa na ghadhabu;+Na moto ukawashwa juu ya Yakobo,+Na hasira pia ikapanda juu ya Israeli.+ 22  Kwa maana hawakuwa na imani katika Mungu,+Wala hawakutegemea wokovu wake.+ 23  Naye akaamuru anga lenye mawingu lililo juu,Naye akaifungua milango ya mbingu.+ 24  Naye akaendelea kuwanyeshea mana ili wale,+Naye akawapa nafaka ya mbinguni.+ 25  Wanadamu walikula mkate wa wenye nguvu;+Aliwapa vyakula mpaka wakashiba.+ 26  Akaanza kufanya upepo wa mashariki uvume mbinguni+Na kufanya upepo wa kusini uvume kwa nguvu zake.+ 27  Naye akawanyeshea chakula kama mavumbi,+Hata viumbe vinavyoruka vyenye mabawa kama chembe za mchanga wa bahari.+ 28  Naye akaendelea kuviangusha katikati ya kambi yake,+Pande zote za maskani zake.+ 29  Nao wakala na kujishibisha sana,+Naye akawaletea walichotamani.+ 30  Hawakuwa wameacha tamaa yao,Chakula chao kilipokuwa kingali kinywani mwao,+ 31  Ndipo ghadhabu ya Mungu ilipopanda juu yao.+Naye akafanya mauaji kati ya wenye nguvu wao;+Na vijana wa Israeli akawaangusha. 32  Ijapokuwa hayo yote walifanya dhambi zaidi+Wala hawakuwa na imani katika kazi zake za ajabu.+ 33  Kwa hiyo akakomesha siku zao kana kwamba ni pumzi tu,+Na miaka yao kwa usumbufu. 34  Kadiri alivyowaua ndivyo pia walivyouliza habari zake,+Nao wakarudi na kumtafuta Mungu.+ 35  Nao wakaanza kukumbuka kwamba Mungu alikuwa Mwamba wao,+Na kwamba Mungu Aliye Juu Zaidi alikuwa Mlipiza-Kisasi wao.+ 36  Nao wakajaribu kumpumbaza kwa kinywa chao;+Na kwa ulimi wao wakajaribu kumwambia uwongo.+ 37  Na moyo wao haukuwa imara kwake;+Nao hawakuwa waaminifu katika agano lake.+ 38  Lakini alikuwa mwenye rehema;+ akawa akilifunika kosa+ wala hakuharibu.+Na mara nyingi akageuzia mbali hasira yake,+Naye akawa haiamshi ghadhabu yake yote. 39  Naye akaendelea kukumbuka kwamba wao ni wenye mwili wa nyama,+Kwamba roho inaenda wala hairudi.+ 40  Jinsi walivyomwasi mara nyingi nyikani,+Wakamhuzunisha jangwani!+ 41  Nao wakawa wakimjaribu Mungu tena na tena,+Nao wakamtia uchungu Mtakatifu wa Israeli.+ 42  Hawakuukumbuka mkono wake,+Ile siku ambayo aliwakomboa kutoka kwa mpinzani,+ 43  Jinsi alivyoweka ishara zake katika Misri+Na miujiza yake katika uwanja wa Soani;+ 44  Na jinsi alivyoanza kubadili mifereji ya Nile iwe damu,+Hivi kwamba hawakuweza kunywa kutoka katika vijito vyao wenyewe.+ 45  Naye akaanza kuwatumia mainzi, ili yapate kuwala;+Na vyura, ili wapate kuwaharibu.+ 46  Naye akaanza kuwapa mende mazao yao,Na kazi yao ngumu akawapa nzige.+ 47  Akauua mzabibu wao kwa mvua ya mawe+Na mikuyu yao kwa mawe ya mvua.+ 48  Naye akawaacha wanyama wao wa kubeba mizigo wapigwe kwa mvua ya mawe+Na mifugo yao kwa homa kali. 49  Akapeleka juu yao hasira yake inayowaka,+Ghadhabu na shutuma na taabu,+Wajumbe wa malaika wanaoleta msiba.+ 50  Akatayarisha njia kwa ajili ya hasira yake.+Hakuzuia nafsi zao zisipatwe na kifo;Nayo maisha yao akayatia kwenye tauni.+ 51  Mwishowe akawapiga na kuwaua wazaliwa wote wa kwanza wa Misri,+Mwanzo wa nguvu zao za uzazi katika mahema ya Hamu.+ 52  Baadaye akawafanya watu wake waondoke kama kondoo,+Na kuwaongoza kama kundi nyikani.+ 53  Naye akaendelea kuwaongoza kwa usalama, wala hawakuhofu kamwe;+Nayo bahari ikawafunika adui zao.+ 54  Naye akawaleta katika eneo lake takatifu,+Eneo hili lenye milima ambalo mkono wake wa kuume ulijipatia.+ 55  Naye akayafukuza mataifa kwa sababu yao,+Na kuwagawia urithi kwa kamba ya kupimia,+Hivi kwamba akayafanya makabila ya Israeli yakae nyumbani kwao wenyewe.+ 56  Nao wakaanza kumjaribu na kumwasi Mungu Aliye Juu Zaidi.+Wala hawakushika vikumbusho vyake.+ 57  Pia wakaendelea kugeuka na kutenda kwa hila kama mababu zao;+Waligeuka huku na huku kama upinde uliolegea.+ 58  Nao wakaendelea kumtia uchungu kwa mahali pao pa juu,+Nao wakaendelea kumchochea awe na wivu kwa sanamu zao za kuchongwa.+ 59  Mungu akasikia,+ akawa na ghadhabu,+Na kwa hiyo akachukia sana Israeli.+ 60  Naye mwishowe akaiacha maskani ya Shilo,+Lile hema ambalo alikaa ndani yake katikati ya watu wa udongo.+ 61  Naye akatia nguvu zake utekwani+Na uzuri wake mkononi mwa mpinzani.+ 62  Naye akaendelea kuwatia watu wake kwenye upanga,+Naye akawa na ghadhabu juu ya urithi wake.+ 63  Moto ukawateketeza wanaume wake vijana,Na mabikira wake hawakusifiwa.+ 64  Nao makuhani wake, wakaangushwa kwa upanga,+Na wajane wao hawakulia.+ 65  Kisha Yehova akaanza kuamka kana kwamba kutoka katika usingizi,+Kama mtu mwenye nguvu akitokwa na ulevi wa divai.+ 66  Naye akaanza kuwapiga adui zake kutoka nyuma;+Akawapa shutuma inayodumu mpaka wakati usio na kipimo.+ 67  Naye akakataa hema la Yosefu;+Na kabila la Efraimu hakulichagua.+ 68  Bali alichagua kabila la Yuda,+Mlima Sayuni, ambao aliupenda.+ 69  Naye akaanza kujenga patakatifu pake kama vilele,+Kama dunia ambayo ameiwekea msingi mpaka wakati usio na kipimo.+ 70  Na kwa hiyo akamchagua Daudi mtumishi wake+Naye akamtoa katika mazizi ya kundi.+ 71  Aache kuwafuata wale wa kike wanaonyonyesha+Akamleta awe mchungaji juu ya Yakobo watu wake+Na juu ya Israeli, urithi wake.+ 72  Naye akaanza kuwachunga kulingana na utimilifu wa moyo wake,+Naye akaanza kuwaongoza kwa ustadi wa mikono yake.+

Maelezo ya Chini