Zaburi 78:1-72
Maskili. Ya Asafu.+
78 Sikilizeni sheria yangu, enyi watu wangu;+Tegeni sikio lenu kwa maneno ya kinywa changu.+
2 Katika neno la kimethali nitakifungua kinywa changu;+Nitafanya vitendawili vya zamani za kale vibubujike,+
3 Ambavyo tumevisikia na tunavijua,+Na ambavyo baba zetu wenyewe wametusimulia;+
4 Ambavyo hatuwafichi wana wao,+Tukivisimulia hata kwa kizazi kitakachokuja,+Sifa za Yehova na nguvu zake+Na mambo yake ya ajabu ambayo amefanya.+
5 Naye akatokeza kikumbusho katika Yakobo,+Na sheria akaiweka katika Israeli,+Mambo ambayo aliwaamuru mababu zetu,+Wawajulishe wana wao;+
6 Ili kizazi kitakachokuja, wana ambao wangezaliwa, wapate kuyajua,+Ili wasimame na kuwasimulia wana wao,+
7 Na kwamba wao watie uhakika wao katika Mungu+Nao wasisahau matendo ya Mungu+ bali washike amri zake.+
8 Nao wasiwe kama mababu zao,+Kizazi chenye ukaidi na chenye kuasi,+Kizazi ambacho hakikuwa kimetayarisha moyo wake+Na ambacho roho yake haikuwa yenye kutegemeka kwa Mungu.+
9 Wana wa Efraimu, wajapokuwa ni wapiga-upinde wenye silaha,+Walirudi nyuma siku ya pigano.+
10 Hawakulishika agano la Mungu,+Nao wakakataa kutembea katika sheria yake.+
11 Pia wakaanza kusahau matendo yake+Na kazi zake za ajabu alizowafanya waone.+
12 Mbele ya mababu zao yeye alikuwa ametenda kwa njia ya ajabu.+Katika nchi ya Misri,+ kiwanja cha Soani.+
13 Aliipasua bahari, ili awaruhusu kuvuka,+Naye akayafanya maji yasimame kama bwawa.+
14 Naye akaendelea kuwaongoza kwa wingu wakati wa mchana+Na usiku kucha kwa nuru ya moto.+
15 Aliipasua miamba nyikani,+Ili awanyweshe kwa wingi kama vilindi vya maji.+
16 Naye akatokeza vijito katika mwamba+Na kufanya maji yateremke kama mito.+
17 Nao wakaendelea kumtendea dhambi hata zaidi+Kwa kumwasi Aliye Juu Zaidi katika eneo lisilo na maji;+
18 Nao wakamjaribu Mungu moyoni mwao+Kwa kuomba chakula kwa ajili ya nafsi yao.+
19 Basi wakaanza kusema vibaya juu ya Mungu.+Walisema: “Je, Mungu anaweza kutayarisha meza nyikani?”+
20 Tazama! Alipiga mwamba+Ili maji yatiririke na mito ifurike.+“Je, anaweza pia kutoa mkate,+Au je, anaweza kuwatayarishia watu wake chakula?”+
21 Ndiyo sababu Yehova alisikia, akaanza kuwa na ghadhabu;+Na moto ukawashwa juu ya Yakobo,+Na hasira pia ikapanda juu ya Israeli.+
22 Kwa maana hawakuwa na imani katika Mungu,+Wala hawakutegemea wokovu wake.+
23 Naye akaamuru anga lenye mawingu lililo juu,Naye akaifungua milango ya mbingu.+
24 Naye akaendelea kuwanyeshea mana ili wale,+Naye akawapa nafaka ya mbinguni.+
25 Wanadamu walikula mkate wa wenye nguvu;+Aliwapa vyakula mpaka wakashiba.+
26 Akaanza kufanya upepo wa mashariki uvume mbinguni+Na kufanya upepo wa kusini uvume kwa nguvu zake.+
27 Naye akawanyeshea chakula kama mavumbi,+Hata viumbe vinavyoruka vyenye mabawa kama chembe za mchanga wa bahari.+
28 Naye akaendelea kuviangusha katikati ya kambi yake,+Pande zote za maskani zake.+
29 Nao wakala na kujishibisha sana,+Naye akawaletea walichotamani.+
30 Hawakuwa wameacha tamaa yao,Chakula chao kilipokuwa kingali kinywani mwao,+
31 Ndipo ghadhabu ya Mungu ilipopanda juu yao.+Naye akafanya mauaji kati ya wenye nguvu wao;+Na vijana wa Israeli akawaangusha.
32 Ijapokuwa hayo yote walifanya dhambi zaidi+Wala hawakuwa na imani katika kazi zake za ajabu.+
33 Kwa hiyo akakomesha siku zao kana kwamba ni pumzi tu,+Na miaka yao kwa usumbufu.
34 Kadiri alivyowaua ndivyo pia walivyouliza habari zake,+Nao wakarudi na kumtafuta Mungu.+
35 Nao wakaanza kukumbuka kwamba Mungu alikuwa Mwamba wao,+Na kwamba Mungu Aliye Juu Zaidi alikuwa Mlipiza-Kisasi wao.+
36 Nao wakajaribu kumpumbaza kwa kinywa chao;+Na kwa ulimi wao wakajaribu kumwambia uwongo.+
37 Na moyo wao haukuwa imara kwake;+Nao hawakuwa waaminifu katika agano lake.+
38 Lakini alikuwa mwenye rehema;+ akawa akilifunika kosa+ wala hakuharibu.+Na mara nyingi akageuzia mbali hasira yake,+Naye akawa haiamshi ghadhabu yake yote.
39 Naye akaendelea kukumbuka kwamba wao ni wenye mwili wa nyama,+Kwamba roho inaenda wala hairudi.+
40 Jinsi walivyomwasi mara nyingi nyikani,+Wakamhuzunisha jangwani!+
41 Nao wakawa wakimjaribu Mungu tena na tena,+Nao wakamtia uchungu Mtakatifu wa Israeli.+
42 Hawakuukumbuka mkono wake,+Ile siku ambayo aliwakomboa kutoka kwa mpinzani,+
43 Jinsi alivyoweka ishara zake katika Misri+Na miujiza yake katika uwanja wa Soani;+
44 Na jinsi alivyoanza kubadili mifereji ya Nile iwe damu,+Hivi kwamba hawakuweza kunywa kutoka katika vijito vyao wenyewe.+
45 Naye akaanza kuwatumia mainzi, ili yapate kuwala;+Na vyura, ili wapate kuwaharibu.+
46 Naye akaanza kuwapa mende mazao yao,Na kazi yao ngumu akawapa nzige.+
47 Akauua mzabibu wao kwa mvua ya mawe+Na mikuyu yao kwa mawe ya mvua.+
48 Naye akawaacha wanyama wao wa kubeba mizigo wapigwe kwa mvua ya mawe+Na mifugo yao kwa homa kali.
49 Akapeleka juu yao hasira yake inayowaka,+Ghadhabu na shutuma na taabu,+Wajumbe wa malaika wanaoleta msiba.+
50 Akatayarisha njia kwa ajili ya hasira yake.+Hakuzuia nafsi zao zisipatwe na kifo;Nayo maisha yao akayatia kwenye tauni.+
51 Mwishowe akawapiga na kuwaua wazaliwa wote wa kwanza wa Misri,+Mwanzo wa nguvu zao za uzazi katika mahema ya Hamu.+
52 Baadaye akawafanya watu wake waondoke kama kondoo,+Na kuwaongoza kama kundi nyikani.+
53 Naye akaendelea kuwaongoza kwa usalama, wala hawakuhofu kamwe;+Nayo bahari ikawafunika adui zao.+
54 Naye akawaleta katika eneo lake takatifu,+Eneo hili lenye milima ambalo mkono wake wa kuume ulijipatia.+
55 Naye akayafukuza mataifa kwa sababu yao,+Na kuwagawia urithi kwa kamba ya kupimia,+Hivi kwamba akayafanya makabila ya Israeli yakae nyumbani kwao wenyewe.+
56 Nao wakaanza kumjaribu na kumwasi Mungu Aliye Juu Zaidi.+Wala hawakushika vikumbusho vyake.+
57 Pia wakaendelea kugeuka na kutenda kwa hila kama mababu zao;+Waligeuka huku na huku kama upinde uliolegea.+
58 Nao wakaendelea kumtia uchungu kwa mahali pao pa juu,+Nao wakaendelea kumchochea awe na wivu kwa sanamu zao za kuchongwa.+
59 Mungu akasikia,+ akawa na ghadhabu,+Na kwa hiyo akachukia sana Israeli.+
60 Naye mwishowe akaiacha maskani ya Shilo,+Lile hema ambalo alikaa ndani yake katikati ya watu wa udongo.+
61 Naye akatia nguvu zake utekwani+Na uzuri wake mkononi mwa mpinzani.+
62 Naye akaendelea kuwatia watu wake kwenye upanga,+Naye akawa na ghadhabu juu ya urithi wake.+
63 Moto ukawateketeza wanaume wake vijana,Na mabikira wake hawakusifiwa.+
64 Nao makuhani wake, wakaangushwa kwa upanga,+Na wajane wao hawakulia.+
65 Kisha Yehova akaanza kuamka kana kwamba kutoka katika usingizi,+Kama mtu mwenye nguvu akitokwa na ulevi wa divai.+
66 Naye akaanza kuwapiga adui zake kutoka nyuma;+Akawapa shutuma inayodumu mpaka wakati usio na kipimo.+
67 Naye akakataa hema la Yosefu;+Na kabila la Efraimu hakulichagua.+
68 Bali alichagua kabila la Yuda,+Mlima Sayuni, ambao aliupenda.+
69 Naye akaanza kujenga patakatifu pake kama vilele,+Kama dunia ambayo ameiwekea msingi mpaka wakati usio na kipimo.+
70 Na kwa hiyo akamchagua Daudi mtumishi wake+Naye akamtoa katika mazizi ya kundi.+
71 Aache kuwafuata wale wa kike wanaonyonyesha+Akamleta awe mchungaji juu ya Yakobo watu wake+Na juu ya Israeli, urithi wake.+
72 Naye akaanza kuwachunga kulingana na utimilifu wa moyo wake,+Naye akaanza kuwaongoza kwa ustadi wa mikono yake.+