Zaburi 49:1-20

Kwa kiongozi. Ya wana wa Kora.+ Muziki. 49  Sikieni hili, enyi vikundi vyote vya watu.Tegeni sikio, enyi wakaaji wote wa mfumo wa mambo,+   Enyi wana wa wanadamu, naam, ninyi wana wa binadamu.Wewe tajiri pamoja nawe maskini.+   Kinywa changu mwenyewe kitasema mambo ya hekima,+Na moyo wangu utatafakari mambo ya uelewaji.+   Nitatega sikio langu nisikie maneno ya kimethali;+Nitafumbua kitendawili+ changu kwa kinubi.   Kwa nini niogope katika siku za uovu,+Wakati ambapo kosa la wanaonipindua linanizingira?+   Wale wanaotegemea riziki zao,+Na ambao wanaendelea kujisifu juu ya wingi wa utajiri wao,+   Hakuna hata mmoja wao anayeweza kumkomboa hata ndugu,+Wala kumpa Mungu fidia kwa ajili yake;   (Nayo bei ya ukombozi wa nafsi yao ni yenye thamani sana+Hivi kwamba imekoma mpaka wakati usio na kipimo)   Hivi kwamba yeye aendelee kuishi milele na asilione shimo.+ 10  Kwa maana yeye huona kwamba hata wenye hekima wanakufa,+Mjinga na asiyetumia akili huangamia wote pamoja,+Nao hulazimika kuwaachia wengine mali yao.+ 11  Tamaa yao ya ndani ni kwamba nyumba zao ziwepo mpaka wakati usio na kipimo,+Maskani zao mpaka kizazi baada ya kizazi.+Wameyaita mashamba yao kwa majina yao.+ 12  Na bado mtu wa udongo, ingawa katika heshima, hawezi kuendelea kukaa;+Kwa kweli analingana na wanyama ambao wameangamizwa.+ 13  Hiyo ndiyo njia ya wale wenye ujinga,+Na ya wale wanaowafuata ambao wanapendezwa na maneno yao wenyewe. Sela. 14  Kama kondoo, wao wamewekewa Kaburi;*+Kifo chenyewe kitawachunga;+Nao wanyoofu watawatawala asubuhi,+Nayo maumbo yao hayatakosa kuchakaa;+Kaburi* badala ya makao yaliyo juu ni kwa ajili ya kila mmoja.+ 15  Hata hivyo, Mungu mwenyewe ataikomboa nafsi yangu kutoka katika mkono wa Kaburi,*+Kwa maana atanipokea. Sela. 16  Usiogope kwa sababu mtu fulani anapata utajiri,+Kwa sababu utukufu wa nyumba yake unaongezeka,+ 17  Kwa maana anapokufa hawezi kuchukua kitu chochote;+Utukufu wake hautashuka chini pamoja naye.+ 18  Kwa maana muda wote wa maisha yake alikuwa akiibariki nafsi yake mwenyewe;+(Na watu watakusifu kwa sababu unajiendeleza vizuri)+ 19  Nafsi yake mwishowe inafikia tu kwenye kizazi cha mababu zake.+Hawataona nuru tena kamwe.+ 20  Mtu wa udongo, ingawa katika heshima, ambaye haelewi,+Kwa kweli analingana na wanyama ambao wameangamizwa.+

Maelezo ya Chini

Sheoli. Tazama Nyongeza 4.
Sheoli. Tazama Nyongeza 4.
Sheoli. Tazama Nyongeza 4.