Zaburi 34:1-22

  • Yehova huwaokoa watumishi wake

    • “Na tulikweze jina lake pamoja” (3)

    • Malaika wa Yehova hulinda (7)

    • “Onjeni mwone kwamba Yehova ni mwema” (8)

    • ‘Hakuna hata mfupa wake mmoja uliovunjwa’ (20)

Wa Daudi, alipojifanya mwenda wazimu+ mbele ya Abimeleki, hivi kwamba akamfukuza, naye akaenda zake. א [Aleph] 34  Nitamsifu Yehova nyakati zote;Sifa yake itakuwa midomoni mwangu daima. ב [Beth]   Nitajigamba* kwa sababu ya Yehova;+Wapole watasikia na kushangilia. ג [Gimel]   Mtukuzeni Yehova pamoja nami;+Na tulikweze jina lake pamoja. ד [Daleth]   Nilimwomba Yehova ushauri, naye akanijibu.+ Aliniokoa kutoka katika mambo yote yanayoniogopesha.+ ה [He]   Wale waliomtazama waling’aa;Nyuso zao hazingeweza kuona aibu. ז [Zayin]   Mtu huyo wa hali ya chini aliita, na Yehova akasikia. Alimwokoa kutoka katika taabu zake zote.+ ח [Heth]   Malaika wa Yehova hupiga kambi pande zote kuwazunguka wanaomwogopa Yeye,+Naye huwaokoa.+ ט [Teth]   Onjeni mwone kwamba Yehova ni mwema;+Mwenye furaha ni mtu anayemkimbilia. י [Yod]   Mwogopeni Yehova, ninyi nyote watakatifu wake,Kwa maana wale wanaomwogopa hawakosi chochote.+ כ [Kaph] 10  Hata wanasimba* wenye nguvu wamelemewa na njaa,Lakini wale wanaomtafuta Yehova hawatakosa chochote chema.+ ל [Lamed] 11  Njooni, wanangu, nisikilizeni;Nitawafundisha kumwogopa Yehova.+ מ [Mem] 12  Ni nani miongoni mwenu anayependa uzimaNa angependa kuishi siku nyingi njema?+ נ [Nun] 13  Basi ulinde ulimi wako usiseme mabaya,+Midomo yako isiseme uwongo.+ ס [Samekh] 14  Acha uovu, utende mema;+Tafuta amani na uifuatie.+ ע [Ayin] 15  Macho ya Yehova yanawatazama waadilifu,+Na masikio yake yanasikiliza kilio chao cha kuomba msaada.+ פ [Pe] 16  Lakini uso wa Yehova uko dhidi ya wale wanaotenda maovu,Ili afutilie mbali kumbukumbu lao lote kutoka duniani.+ צ [Tsade] 17  Walilia kwa sauti, na Yehova akasikia;+Aliwaokoa kutoka katika taabu zao zote.+ ק [Qoph] 18  Yehova yuko karibu na wale waliovunjika moyo;+Huwaokoa waliopondeka roho.*+ ר [Resh] 19  Mwadilifu ana matatizo mengi,*+Lakini Yehova humwokoa kutoka katika matatizo hayo yote.+ ש [Shin] 20  Anailinda mifupa yake yote;Haujavunjwa hata mmoja.+ ת [Taw] 21  Msiba utamuua mwovu;Wale wanaomchukia mwadilifu watahesabiwa kuwa na hatia. 22  Yehova anaukomboa uhai wa* watumishi wake;Hakuna yeyote anayemkimbilia atakayepatikana na hatia.+

Maelezo ya Chini

Au “Nafsi yangu itajigamba.”
Au “wanasimba wenye manyoya marefu shingoni ambao ni.”
Au “waliovunjika moyo.”
Au “misiba mingi.”
Au “anaikomboa nafsi ya.”