Zaburi 95:1-11
95 Njooni, na tumshangilie Yehova kwa sauti!
Na tumpazie sauti kwa ushindi Mwamba wetu wa wokovu.+
2 Twendeni mbele zake* tukiwa na shukrani;+Na tuimbe na kumpazia sauti kwa ushindi.
3 Kwa maana Yehova ni Mungu mkuu,Mfalme mkuu juu ya miungu mingine yote.+
4 Sehemu zenye kina za dunia zimo mkononi mwake;Vilele vya milima ni vyake.+
5 Bahari, ambayo aliiumba, ni yake,+Na mikono yake ilitengeneza nchi kavu.+
6 Njooni, tuabudu na kuinama;Na tupige magoti mbele za Yehova Muumba wetu.+
7 Kwa maana yeye ni Mungu wetu,Na sisi ni watu wa malisho yake,Kondoo anaowatunza.*+
Leo ikiwa mtaisikiliza sauti yake,+
8 Msiufanye moyo wenu kuwa mgumu kama mlivyofanya kule Meriba,*+Kama katika siku ya Masa* kule nyikani,+
9 Mababu zenu waliponijaribu;+Walinipima, ingawa walikuwa wameona matendo yangu.+
10 Kwa miaka 40 nilichukizwa na kizazi hicho, nikasema:
“Wao ni watu wanaopotoka sikuzote katika mioyo yao;Hawajazijua njia zangu.”
11 Kwa hiyo niliapa kwa hasira yangu:
“Hawataingia katika pumziko langu.”+
Maelezo ya Chini
^ Tnn., “mbele za uso wake.”
^ Tnn., “wa mkono wake.”
^ Maana yake “Kugombana.”
^ Maana yake “Kujaribu; Jaribu.”