Zaburi 45:1-17
Kwa kiongozi; umepatanishwa na mtindo wa “Mayungiyungi.” Wa wana wa Kora.+ Maskili.* Wimbo wa upendo.
45 Moyo wangu umesisimuliwa na jambo jema.
Ninasema: “Wimbo wangu unamhusu* mfalme.”+
Ulimi wangu na uwe kalamu+ ya mnakili* stadi.+
2 Una sura nzuri kuliko wanadamu wote.
Maneno yenye fadhili hutiririka kutoka katika midomo yako.+
Ndiyo sababu Mungu amekubariki milele.+
3 Jifunge upanga wako+ pajani, Ee mwenye nguvu,+Katika heshima na fahari yako.+
4 Na katika fahari yako endelea mpaka ushinde;*+Panda utetee kweli na unyenyekevu na uadilifu,+Na mkono wako wa kulia utatimiza* mambo yanayoogopesha.
5 Mishale yako ni mikali, inaangusha mataifa mbele yako;+Inachoma mioyo ya maadui wa mfalme.+
6 Mungu ni kiti chako cha ufalme milele na milele;+Fimbo ya ufalme wako ni fimbo ya unyoofu.*+
7 Ulipenda uadilifu+ na kuchukia uovu.+
Ndiyo sababu Mungu, Mungu wako, amekutia mafuta+ kwa mafuta ya kushangilia+ kuliko wenzako.
8 Mavazi yako yote yametiwa manukato ya manemane na udi na kida;Kutoka katika jumba tukufu la mfalme lililotengenezwa kwa pembe za tembo, vinanda vinakufanya ushangilie.
9 Mabinti wa wafalme ni miongoni mwa wanawake wako wanaoheshimiwa.
Malkia amesimama mkono wako wa kulia, akiwa amepambwa kwa dhahabu ya Ofiri.+
10 Sikiliza, Ee binti, sikiliza kwa makini na utege sikio lako;Wasahau watu wako na nyumba ya baba yako.
11 Naye mfalme atautamani urembo wako,Kwa maana yeye ni bwana wako,Kwa hiyo mwinamie.
12 Binti ya Tiro ataleta zawadi;Watu matajiri zaidi watatafuta kibali chako.*
13 Katika jumba la mfalme,* binti ya mfalme ana utukufu mwingi ajabu;Mavazi yake yamepambwa kwa* dhahabu.
14 Atapelekwa kwa mfalme akiwa na mavazi yaliyofumwa kwa ustadi mkubwa.*
Mabikira wenzake wanaomfuata wanaletwa ndani mbele ya mfalme.
15 Wataletwa kwa furaha na shangwe;Wataingia katika jumba la mfalme.
16 Wana wako watachukua mahali pa mababu zako.
Utawaweka kuwa wakuu katika dunia yote.+
17 Nitalitangaza jina lako katika vizazi vyote vijavyo.+
Ndiyo sababu mataifa yatakusifu milele na milele.
Maelezo ya Chini
^ Tnn., “Kazi zangu zinamhusu.”
^ Au “mwandishi.”
^ Tnn., “utakufundisha.”
^ Au “ufanikiwe.”
^ Au “haki.”
^ Au “watautuliza uso wako.”
^ Tnn., “Ndani.”
^ Tnn., “yametiwa mapambo ya.”
^ Au labda, “kwa majoho yaliyotariziwa.”