Zaburi 119:1-176
-
Kulithamini neno la Mungu lenye thamani
א [Aleph]
119 Wenye furaha ni wale wasio na lawama* katika njia yao,Wanaotembea katika sheria ya Yehova.+
2 Wenye furaha ni wale wanaoshika vikumbusho vyake,+Wanaomtafuta kwa moyo wao wote.+
3 Hawatendi uovu wowote;Wanatembea katika njia zake.+
4 UmeamuruKwamba maagizo yako yafuatwe kwa uangalifu.+
5 Laiti ningeweza kubaki imara*+Ili niyashike masharti yako!
6 Ndipo sitaaibishwa+Ninapokazia uangalifu amri zako zote.
7 Nitakusifu kwa moyo mnyoofuNinapojifunza hukumu zako za uadilifu.
8 Nitayashika masharti yako.
Kamwe usiniache kabisa.
ב [Beth]
9 Kijana anaweza kuisafishaje njia yake?
Kwa kujilinda kulingana na neno lako.+
10 Ninakutafuta kwa moyo wangu wote.
Usiache nikengeuke kutoka katika amri zako.+
11 Ninaweka neno lako moyoni mwangu kama hazina+Ili nisikutendee dhambi.+
12 Na usifiwe, Ee Yehova;Nifundishe masharti yako.
13 Kwa midomo yangu ninatangazaHukumu zote ulizonena.
14 Ninashangilia kwa sababu ya vikumbusho vyako+Kuliko vitu vingine vyote vyenye thamani.+
15 Nitatafakari* maagizo yako+Na kuzikazia macho njia zako.+
16 Ninazipenda sana sheria zako.
Sitalisahau neno lako.+
ג [Gimel]
17 Nitendee kwa fadhili mimi mtumishi wako,Ili niishi na kulishika neno lako.+
18 Yafumbue macho yangu ili nione waziMambo yanayostaajabisha katika sheria yako.
19 Mimi ni mgeni tu nchini.+
Usinifiche amri zako.
20 Ninapondeka* kwa kutamani sanaHukumu zako nyakati zote.
21 Unawakemea wenye kimbelembele,Watu waliolaaniwa wanaokengeuka kutoka katika amri zako.+
22 Niondolee* dhihaka na dharau,Kwa maana nimeshika vikumbusho vyako.
23 Hata wakuu wanapoketi pamoja na kusema mambo mabaya kunihusu,Mimi mtumishi wako ninatafakari* masharti yako.
24 Ninavipenda sana vikumbusho vyako;+Navyo ni washauri wangu.+
ד [Daleth]
25 Ninalala kifudifudi mavumbini.+
Nihifadhi hai kulingana na neno lako.+
26 Nilikwambia kuhusu njia zangu, nawe ukanijibu;Nifundishe masharti yako.+
27 Nifanye nielewe maana* ya maagizo yako,Ili niweze kutafakari* kazi zako zinazostaajabisha.+
28 Nimekosa usingizi kwa sababu ya huzuni.
Nitie nguvu kulingana na neno lako.
29 Niondolee njia ya udanganyifu,+Na unionyeshe kibali kwa kunipa sheria yako.
30 Nimechagua njia ya uaminifu.+
Ninatambua kwamba hukumu zako zinafaa.
31 Ninashikamana na vikumbusho vyako.+
Ee Yehova, usiache nikatishwe tamaa.*+
32 Nitaifuata kwa bidii* njia ya amri zakoKwa sababu wewe huufanya moyo wangu uwe na nafasi kwa ajili yake.*
ה [He]
33 Nifundishe, Ee Yehova,+ njia ya masharti yako,Nami nitaifuata mpaka mwisho.+
34 Nipe uelewaji,Ili niweze kushika sheria yakoNa kuitii kwa moyo wangu wote.
35 Niongoze* katika njia ya amri zako,+Kwa maana ninapendezwa nayo.
36 Uelekeze moyo wangu kwenye vikumbusho vyako,Wala si kwa tamaa ya* kichoyo.+
37 Yageuzie mbali macho yangu yasitazame mambo yasiyofaa;+Nihifadhi hai katika njia yako.
38 Nitimizie mimi mtumishi wako ahadi yako,*Ili uogopwe.*
39 Niondolee aibu ninayoogopa sana,Kwa maana hukumu zako ni njema.+
40 Tazama jinsi ninavyoyatamani sana maagizo yako!
Nihifadhi hai katika uadilifu wako.
ו [Waw]
41 Acha nijionee upendo wako mshikamanifu, Ee Yehova,+Wokovu wako kulingana na ahadi yako;*+
42 Kisha nitamjibu yule anayenidhihaki,Kwa maana ninalitumaini neno lako.
43 Usiondoe kabisa neno la kweli kutoka kinywani mwangu,Kwa maana nimetumaini* hukumu yako.
44 Nitaishika sheria yako daima,Milele na milele.+
45 Nami nitatembeatembea mahali salama,*+Kwa maana ninayatafuta maagizo yako.
46 Nitaongea kuhusu vikumbusho vyako mbele ya wafalme,Nami sitaaibika.+
47 Ninazipenda sana amri zako,Naam, ninazipenda.+
48 Nitainua mikono yangu kuelekea amri zako, ambazo ninazipenda,+Nami nitayatafakari* masharti yako.+
ז [Zayin]
49 Likumbuke neno lako ulilomwambia* mtumishi wako,Ambalo kupitia hilo unanipa tumaini.*
50 Hilo ndilo faraja yangu katika mateso yangu,+Kwa maana neno lako limenihifadhi hai.
51 Wenye kimbelembele wananidhihaki sana,Lakini sikengeuki kutoka kwenye sheria yako.+
52 Ninazikumbuka hukumu zako za tangu zamani,+ Ee Yehova,Nazo zinanifariji.+
53 Nimeshikwa na hasira kali kwa sababu ya waovu,Wanaoiacha sheria yako.+
54 Masharti yako ni nyimbo kwanguPopote ninapoishi.*
55 Wakati wa usiku ninalikumbuka jina lako, Ee Yehova,+Ili niweze kuishika sheria yako.
56 Nimezoea kufanya hivyoKwa sababu nimeyatii maagizo yako.
ח [Heth]
57 Yehova ni fungu langu;+Nimeahidi kuyashika maneno yako.+
58 Ninakusihi* kwa moyo wangu wote;+Nionyeshe kibali+ kulingana na ahadi yako.*
59 Nimezichunguza njia zangu,Ili niirudishe miguu yangu kwenye vikumbusho vyako.+
60 Ninafanya haraka wala sikawiiKuzishika amri zako.+
61 Kamba za waovu zinanizunguka,Lakini siisahau sheria yako.+
62 Katikati ya usiku ninaamka ili kukushukuru+Kwa sababu ya hukumu zako za uadilifu.
63 Mimi ni rafiki ya wote wanaokuogopa weweNa ya wale wanaoyatii maagizo yako.+
64 Upendo wako mshikamanifu, Ee Yehova, umeijaza dunia;+Nifundishe masharti yako.
ט [Teth]
65 Umenitendea mema mimi mtumishi wako,Ee Yehova, kulingana na neno lako.
66 Nifundishe busara na ujuzi,+Kwa maana nimezitumaini amri zako.
67 Kabla ya kuteswa, nilikuwa nikikengeuka,*Lakini sasa ninalishika neno lako.+
68 Wewe ni mwema+ na kazi zako ni njema.
Nifundishe masharti yako.+
69 Wenye kimbelembele hunipaka uwongo,Lakini ninayatii maagizo yako kwa moyo wangu wote.
70 Moyo wao umekufa ganzi,*+Lakini ninaipenda sana sheria yako.+
71 Ni vema kwamba nimeteswa,+Ili nijifunze masharti yako.
72 Sheria uliyotangaza ni njema kwangu,+Kuliko maelfu ya vipande vya dhahabu na fedha.+
י [Yod]
73 Mikono yako iliniumba na kunifinyanga.
Nipe uelewaji,Ili nijifunze amri zako.+
74 Wale wanaokuogopa huniona na kushangilia,Kwa maana neno lako ni tumaini langu.*+
75 Ninajua, Ee Yehova, kwamba hukumu zako ni za uadilifu+Na kwamba umenitesa kwa uaminifu wako.+
76 Tafadhali, upendo wako mshikamanifu+ na unifariji,Kulingana na ahadi yako uliyonipa* mimi mtumishi wako.
77 Nionyeshe rehema ili niendelee kuishi,+Kwa maana ninaipenda sana sheria yako.+
78 Wenye kimbelembele na waaibishwe,Kwa maana wananikosea bila sababu.*
Lakini nitayatafakari* maagizo yako.+
79 Acha wale wanaokuogopa warudi kwangu,Wale wanaojua vikumbusho vyako.
80 Moyo wangu na uwe bila lawama katika kufuata masharti yako,+Ili nisiaibishwe.+
כ [Kaph]
81 Ninautamani sana wokovu wako,+Kwa maana neno lako ni tumaini langu.*
82 Macho yangu yanatamani sana neno lako+Huku nikisema: “Utanifariji lini?”+
83 Kwa maana mimi ni kama kiriba cha ngozi kilichokaushwa na moshi,Lakini siyasahau masharti yako.+
84 Mimi mtumishi wako nisubiri kwa siku ngapi?
Ni lini utakapowahukumu wale wanaonitesa?+
85 Wenye kimbelembele wananichimbia mashimo,Wale wanaoasi sheria yako.
86 Amri zako zote zinategemeka.
Watu wananitesa bila sababu; nisaidie!+
87 Karibu waniangamize kutoka duniani,Lakini sikuyaacha maagizo yako.
88 Nihifadhi hai kwa sababu ya upendo wako mshikamanifu,Ili nishike vikumbusho ulivyosema.
ל [Lamed]
89 Milele, Ee Yehova,Neno lako litadumu mbinguni.+
90 Uaminifu wako umekuwepo kwa vizazi vyote.+
Umeiimarisha kabisa dunia, ili idumu.+
91 Kwa sababu ya hukumu zako zinadumu* mpaka leo,Kwa maana zote ni watumishi wako.
92 Kama singeipenda sana sheria yako,Ningekuwa nimeangamia katika mateso yangu.+
93 Sitayasahau kamwe maagizo yako,Kwa sababu kupitia hayo umenihifadhi hai.+
94 Mimi ni wako; niokoe,+Kwa sababu nimeyatafuta maagizo yako.+
95 Waovu wanasubiri kuniangamiza,Lakini ninavikazia sana fikira vikumbusho vyako.
96 Nimeona mwisho wa ukamilifu wote,Lakini amri yako haina mpaka.*
מ [Mem]
97 Jinsi ninavyoipenda sana sheria yako!+
Ninaitafakari* mchana kutwa.+
98 Amri yako hunifanya niwe na hekima kuliko maadui wangu,+Kwa sababu ninayo milele.
99 Nina ufahamu mwingi kuliko walimu wangu wote,+Kwa sababu ninavitafakari* vikumbusho vyako.
100 Ninatenda kwa uelewaji mwingi kuliko wanaume wazee,Kwa sababu ninayatii maagizo yako.
101 Ninakataa kutembea kwenye njia yoyote ya uovu,+Ili nishike neno lako.
102 Sigeuki kando kutoka katika hukumu zako,Kwa maana umenifundisha.
103 Jinsi maneno yako yalivyo matamu kwenye kaakaa langu,Kuliko asali kinywani mwangu!+
104 Kwa sababu ya maagizo yako ninatenda kwa uelewaji.+
Ndiyo sababu ninaichukia kila njia ya uwongo.+
נ [Nun]
105 Neno lako ni taa ya mguu wangu,Na nuru ya njia yangu.+
106 Nimeweka kiapo, nami nitakitimiza,Kwamba nitazishika hukumu zako za uadilifu.
107 Nimeteseka sana.+
Ee Yehova, nihifadhi hai kulingana na neno lako.+
108 Tafadhali yafurahie matoleo yangu ya hiari ya kukusifu,*+ Ee Yehova,Na unifundishe hukumu zako.+
109 Uhai wangu umo hatarini daima,*Lakini sijaisahau sheria yako.+
110 Waovu wamenitegea mtego,Lakini sijakengeuka kutoka katika maagizo yako.+
111 Ninavichukua vikumbusho vyako kuwa mali yangu ya kudumu,*Kwa maana hivyo ni shangwe ya moyo wangu.+
112 Nimeazimia* kuyatii masharti yakoNyakati zote, mpaka mwisho.
ס [Samekh]
113 Ninawachukia watu wenye moyo nusunusu,*+Lakini ninaipenda sheria yako.+
114 Wewe ni mahali pangu pa kujificha na ngao yangu,+Kwa maana neno lako ni tumaini langu.*+
115 Kaeni mbali nami, enyi waovu,+Ili nizishike amri za Mungu wangu.
116 Nitegemeze kama ulivyoahidi,*+Ili niendelee kuishi;Usiache tumaini langu libadilike na kunikatisha tamaa.*+
117 Nitegemeze ili niokolewe;+Kisha nitayakazia uangalifu daima masharti yako.+
118 Unawakataa wote wanaokengeuka kutoka katika masharti yako,+Kwa maana ni waongo na wadanganyifu.
119 Unawatupilia mbali waovu wote walio duniani kana kwamba ni takataka.*+
Ndiyo sababu ninavipenda vikumbusho vyako.
120 Mwili wangu unatetemeka kwa sababu ya kukuhofu;Ninaogopa hukumu zako.
ע [Ayin]
121 Nimetenda yaliyo ya haki na uadilifu.
Usiniache mikononi mwa wale wanaonikandamiza!
122 Nihakikishie hali njema mimi mtumishi wako;Wenye kimbelembele wasinikandamize.
123 Macho yangu yamechoka nikiungojea wokovu wako+Na ahadi yako ya* uadilifu.+
124 Nitendee mimi mtumishi wako kwa upendo mshikamanifu,+Na unifundishe masharti yako.+
125 Mimi ni mtumishi wako; nipe uelewaji,+Ili nijue vikumbusho vyako.
126 Wakati umefika wa Yehova kutenda,+Kwa maana wameivunja sheria yako.
127 Ndiyo sababu ninazipenda amri zakoKuliko dhahabu, hata dhahabu bora.*+
128 Kwa hiyo, ninayaona mafundisho* yote yanayotoka kwako kuwa yanafaa;+Ninaichukia kila njia ya uwongo.+
פ [Pe]
129 Vikumbusho vyako ni vizuri sana.
Ndiyo sababu ninavishika.
130 Kufunuliwa kwa maneno yako huleta nuru,+Na humpa uelewaji mtu asiye na uzoefu.+
131 Ninakifumbua wazi kinywa changu na kutweta,*Kwa sababu ninazitamani sana amri zako.+
132 Nigeukie na kunionyesha kibali,+Kama unavyowatendea* wale wanaolipenda jina lako.+
133 Ziongoze hatua zangu kwa usalama* kupitia neno lako;Jambo lolote ovu lisinitawale.+
134 Niokoe* kutoka kwa wanadamu wanaokandamiza,Nami nitayatii maagizo yako.
135 Ufanye uso wako uniangazie* mimi mtumishi wako,+Na unifundishe masharti yako.
136 Macho yangu yanatiririkwa na machoziKwa sababu watu hawatii sheria yako.+
צ [Tsade]
137 Wewe ni mwadilifu, Ee Yehova,+Na hukumu zako ni za haki.+
138 Vikumbusho unavyotoa ni vya uadilifuNavyo vinategemeka kabisa.
139 Bidii yangu inanila,+Kwa sababu maadui wangu wameyasahau maneno yako.
140 Neno lako ni safi kabisa,+Nami mtumishi wako ninalipenda.+
141 Mimi ni duni na mwenye kudharauliwa;+Hata hivyo, sijayasahau maagizo yako.
142 Uadilifu wako ni uadilifu wa milele,+Na sheria yako ni kweli.+
143 Hata nikipatwa na taabu na shida,Nitaendelea kuzipenda sana amri zako.
144 Uadilifu wa vikumbusho vyako ni wa milele.
Nipe uelewaji,+ ili niendelee kuishi.
ק [Qoph]
145 Ninakuita kwa moyo wangu wote. Nijibu, Ee Yehova.
Nitayashika masharti yako.
146 Ninakulilia wewe; niokoe!
Nitashika vikumbusho vyako.
147 Nimeamka kabla ya mapambazuko* ili nililie msaada,+Kwa maana maneno yako ni tumaini langu.*
148 Macho yangu hufunguka kabla ya makesha ya usiku,Ili nitafakari* neno lako.+
149 Isikie sauti yangu kwa sababu ya upendo wako mshikamanifu.+
Ee Yehova, nihifadhi hai kulingana na haki yako.
150 Watu wenye mwenendo wa aibu* hunikaribia;Wako mbali sana na sheria yako.
151 Wewe uko karibu nami, Ee Yehova,+Na amri zako zote ni kweli.+
152 Zamani za kale nilijifunza kuhusu vikumbusho vyako,Ambavyo umeviweka vidumu milele.+
ר [Resh]
153 Yatazame mateso yangu na uniokoe,+Kwa maana sijaisahau sheria yako.
154 Nitetee* na uniokoe;+Nihifadhi hai kulingana na ahadi yako.*
155 Wokovu uko mbali sana na waovu,Kwa maana hawajayatafuta masharti yako.+
156 Rehema zako ni nyingi, Ee Yehova.+
Nihifadhi hai kulingana na haki yako.
157 Wanaonitesa na pia maadui wangu ni wengi;+Lakini sijakengeuka kutoka katika vikumbusho vyako.
158 Ninawatazama wenye hila kwa chuki kali,Kwa sababu hawalishiki neno lako.+
159 Tazama jinsi ninavyoyapenda sana maagizo yako!
Ee Yehova, nihifadhi hai kwa sababu ya upendo wako mshikamanifu.+
160 Kiini hasa cha neno lako ni kweli,+Na hukumu zako zote za uadilifu zinadumu milele.
ש [Sin] au [Shin]
161 Wakuu wananitesa+ bila sababu,Lakini moyo wangu unayahofu maneno yako.+
162 Ninashangilia kwa sababu ya neno lako+Kama mtu anayepata nyara nyingi.
163 Nauchukia uwongo—nauchukia sana+—Ninaipenda sheria yako.+
164 Mara saba kwa siku ninakusifu weweKwa sababu ya hukumu zako za uadilifu.
165 Wale wanaoipenda sheria yako wana amani nyingi;+Hakuna chochote kinachoweza kuwakwaza.*
166 Ninayatazamia matendo yako ya wokovu, Ee Yehova,Nami ninazishika amri zako.
167 Ninavishika vikumbusho vyako,Nami navipenda sana.+
168 Ninayatii maagizo yako na vikumbusho vyako,Kwa maana unajua mambo yote ninayotenda.+
ת [Taw]
169 Kilio changu cha kuomba msaada na kikufikie wewe, Ee Yehova.+
Nifanye nielewe, kulingana na neno lako.+
170 Ombi langu la kutaka kibali na lifike mbele zako.
Niokoe, kama ulivyoahidi.*
171 Midomo yangu na ifurikwe na sifa,+Kwa maana wewe hunifundisha masharti yako.
172 Ulimi wangu na uimbe kuhusu neno lako,+Kwa maana amri zako zote ni za uadilifu.
173 Mkono wako na uwe tayari kunisaidia,+Kwa sababu nimechagua kutii maagizo yako.+
174 Ninautamani sana wokovu wako, Ee Yehova,Nami ninaipenda sana sheria yako.+
175 Acha niishi ili nikusifu;+Hukumu zako na ziwe msaada wangu.
176 Nimetangatanga kama kondoo aliyepotea.+ Nitafute mimi mtumishi wako,Kwa maana sijazisahau amri zako.+
Maelezo ya Chini
^ Au “wanaoshika utimilifu.”
^ Tnn., “Laiti njia zangu zingekuwa zimeimarishwa kabisa.”
^ Au “Nitajifunza.”
^ Au “Nafsi yangu inapondeka.”
^ Tnn., “Vingirisha mbali nami.”
^ Au “ninajifunza.”
^ Tnn., “njia.”
^ Au “kujifunza.”
^ Au “niaibishwe.”
^ Tnn., “Nitakimbia katika.”
^ Au labda, “huufanya moyo wangu uwe na ujasiri.”
^ Au “Nitembeze.”
^ Au “kwa faida za.”
^ Au “neno lako.”
^ Au labda, “Ambayo hutolewa kwa wale wanaokuogopa.”
^ Au “neno lako.”
^ Au “ninangojea.”
^ Au “mahali penye nafasi kubwa.”
^ Au “nitajifunza.”
^ Au “Kumbuka ahadi yako uliyompa.”
^ Au “Ambalo ulinifanya nisubiri.”
^ Au “Katika nyumba ninamoishi kama mgeni.”
^ Au “Ninautuliza (ninatafuta tabasamu ya) uso wako.”
^ Au “neno lako.”
^ Au “nilikuwa nikitenda dhambi bila kukusudia.”
^ Tnn., “hauna hisia, ni kama mafuta.”
^ Au “ninalingojea neno lako.”
^ Au “neno lako ulilonipa.”
^ Au labda, “kwa kusema uwongo.”
^ Au “nitajifunza.”
^ Au “ninalingojea neno lako.”
^ Yaani, kazi zake zote za uumbaji.
^ Tnn., “ni pana sana.”
^ Au “Ninajifunza kuihusu.”
^ Au “ninajifunza.”
^ Tnn., “matoleo ya hiari ya kinywa changu.”
^ Au “Nafsi yangu imo mikononi mwangu daima.”
^ Au “urithi wangu wa milele.”
^ Tnn., “Nimeuelekeza moyo wangu.”
^ Au “moyo uliogawanyika.”
^ Au “Ninalingojea neno lako.”
^ Au “kulingana na neno lako.”
^ Au “liaibishwe.”
^ Neno la Kiebrania linalotafsiriwa “takataka” katika mstari huu linarejelea uchafu unaotoka katika fedha au dhahabu inapoyeyushwa.
^ Au “neno lako la.”
^ Au “iliyosafishwa.”
^ Au “maagizo.”
^ Tnn., “kuhemahema.”
^ Tnn., “Kulingana na uamuzi wako kuwaelekea.”
^ Au “Zifanye hatua zangu ziwe imara.”
^ Tnn., “Nikomboe.”
^ Au “utabasamu kunielekea.”
^ Au “alfajiri.”
^ Au “Ninayangojea maneno yako.”
^ Au “nijifunze.”
^ Au “mwenendo mpotovu.”
^ Au “Iendeshe kesi yangu.”
^ Au “neno lako.”
^ Au “Hakuna cha kuwakwaza.”
^ Au “kulingana na neno lako.”