Zaburi 123:1-4
Wimbo wa Safari za Kupanda.
123 Nayainua macho yangu kukuelekea wewe,+Wewe unayeketi kwenye kiti cha ufalme mbinguni.
2 Kama macho ya watumishi yanavyoutazama mkono wa bwana wao,Na macho ya kijakazi yanavyoutazama mkono wa bimkubwa wake,Ndivyo macho yetu yanavyokutazama wewe, Ee Yehova Mungu wetu+Mpaka utakapotuonyesha kibali.+
3 Tuonyeshe kibali, Ee Yehova, tuonyeshe kibali,Kwa maana tumedharauliwa vya kutosha.+
4 Tumedhihakiwa vya kutosha na* watu wanaojitumainiNa kudharauliwa na wenye kiburi.
Maelezo ya Chini
^ Au “Nafsi yetu imechoshwa na dhihaka nyingi za.”