Zaburi 123:1-4

  • Kumtazama Yehova ili kupata kibali

    • ‘Kama watumishi, tunamtazama Yehova’ (2)

    • “Tumedharauliwa vya kutosha” (3)

Wimbo wa Safari za Kupanda. 123  Nayainua macho yangu kukuelekea wewe,+Wewe unayeketi kwenye kiti cha ufalme mbinguni.   Kama macho ya watumishi yanavyoutazama mkono wa bwana wao,Na macho ya kijakazi yanavyoutazama mkono wa bimkubwa wake,Ndivyo macho yetu yanavyokutazama wewe, Ee Yehova Mungu wetu+Mpaka utakapotuonyesha kibali.+   Tuonyeshe kibali, Ee Yehova, tuonyeshe kibali,Kwa maana tumedharauliwa vya kutosha.+   Tumedhihakiwa vya kutosha na* watu wanaojitumainiNa kudharauliwa na wenye kiburi.

Maelezo ya Chini

Au “Nafsi yetu imechoshwa na dhihaka nyingi za.”