Zaburi 105:1-45

  • Matendo ya uaminifu ya Yehova kuelekea watu wake

    • Mungu anakumbuka agano lake (8-10)

    • “Msiwaguse watiwa-mafuta wangu” (15)

    • Yosefu aliye utumwani atumiwa na Mungu (17-22)

    • Miujiza ya Mungu nchini Misri (23-36)

    • Waisraeli watoka Misri (37-39)

    • Mungu akumbuka agano alilofanya pamoja na Abrahamu (42)

105  Mshukuruni Yehova,+ liitieni jina lake,Yajulisheni mataifa matendo yake!+   Mwimbieni, mwimbieni sifa,*Tafakarini* kazi zake zote zinazostaajabisha.+   Jivunieni jina lake takatifu.+ Mioyo ya wale wanaomtafuta Yehova na ishangilie.+   Mtafuteni Yehova+ na nguvu zake. Utafuteni uso* wake daima.   Kumbukeni kazi zinazostaajabisha alizofanya,Miujiza yake na hukumu alizotangaza,+   Enyi uzao wa* Abrahamu mtumishi wake,+Enyi wana wa Yakobo, watu wake aliowachagua.+   Yeye ni Yehova Mungu wetu.+ Hukumu zake ziko duniani kote.+   Anakumbuka agano lake milele,+Ahadi aliyotoa,* hata kufikia vizazi elfu,+   Agano alilofanya na Abrahamu,+Na kiapo alichomwapia Isaka,+ 10  Alichotoa kama amri kwa YakoboNa kama agano la kudumu kwa Israeli, 11  Akisema, “Nitakupa nchi ya Kanaani+Kuwa urithi wako uliogawiwa.”+ 12  Wakati walipokuwa wachache,+Naam, wachache sana, nao walikuwa wageni nchini.+ 13  Walitembeatembea kutoka taifa moja hadi taifa lingine,Kutoka ufalme mmoja hadi ufalme mwingine.+ 14  Hakumruhusu mtu yeyote awakandamize,+Lakini kwa sababu yao aliwakaripia wafalme,+ 15  Akisema, “Msiwaguse watiwa-mafuta wangu,Wala msiwatendee manabii wangu jambo lolote baya.”+ 16  Alileta njaa kali nchini;+Alifanya wakose mikate.* 17  Alimtuma mtu awatangulieAmbaye aliuzwa kuwa mtumwa, Yosefu.+ 18  Waliifunga* miguu yake kwa pingu,+Shingo yake ilitiwa katika vyuma;* 19  Mpaka wakati ambapo neno lake lilitimia,+Neno la Yehova ndilo lililomsafisha. 20  Mfalme aliamuru afunguliwe,+Mtawala wa mataifa akamweka huru. 21  Akamweka kuwa bwana mkubwa wa nyumba yake,Mtawala wa mali zake zote,+ 22  Ili awe na mamlaka juu ya* wakuu wake kama alivyopenda*Na kuwafundisha wazee wake hekima.+ 23  Kisha Israeli akaja Misri,+Na Yakobo akakaa akiwa mgeni katika nchi ya Hamu. 24  Mungu aliwafanya watu wake waongezeke sana;+Aliwafanya wawe na nguvu kuliko maadui wao,+ 25  Akaruhusu mioyo yao ibadilike ili wawachukie watu wake,Ili wapange njama dhidi ya watumishi wake.+ 26  Alimtuma Musa mtumishi wake,+Na Haruni,+ aliyekuwa amemchagua. 27  Walifanya ishara zake kati yao,Miujiza yake katika nchi ya Hamu.+ 28  Alilituma giza na nchi ikawa giza;+Hawakuasi maneno yake. 29  Alibadili maji yao yakawa damuNa kuwaua samaki wao.+ 30  Nchi yao ikajaa vyura,+Hata katika vyumba vya mfalme. 31  Aliagiza nzi wavamieNa mbu* katika maeneo yao yote.+ 32  Aliibadili mvua yao ikawa mvua ya maweNaye akatuma radi* katika nchi yao.+ 33  Aliipiga mizabibu yao na mitini yaoNa kuivunjavunja miti ya eneo lao. 34  Aliagiza nzige wavamie,Nzige wachanga wasio na idadi.+ 35  Walikula kabisa mimea yote nchini,Nao wakala kabisa mazao ya ardhi. 36  Kisha akamuua kila mzaliwa wa kwanza katika nchi yao,+Mwanzo wa nguvu zao za uzazi. 37  Aliwatoa nje watu wake wakiwa na fedha na dhahabu;+Na hakuna yeyote katika makabila yake aliyejikwaa. 38  Misri ilishangilia walipoondoka,Kwa maana hofu ya Israeli* ilikuwa imewashika.+ 39  Alitandaza wingu ili liwafunike+Na moto uangaze wakati wa usiku.+ 40  Waliomba, naye akaleta kware;+Aliendelea kuwashibisha mkate kutoka mbinguni.+ 41  Alifungua mwamba, maji yakatiririka kutoka humo;+Maji hayo yalitiririka jangwani kama mto.+ 42  Kwa maana aliikumbuka ahadi takatifu aliyompa Abrahamu mtumishi wake.+ 43  Kwa hiyo akawatoa watu wake wakishangilia,+Watu wake aliowachagua aliwatoa kwa kilio cha shangwe. 44  Aliwapa nchi za mataifa;+Walirithi vitu ambavyo mataifa mengine yalikuwa yametaabika kuvipata,+ 45  Ili waweze kutii maagizo yake+Na kushika sheria zake. Msifuni Yah!*

Maelezo ya Chini

Au labda, “Zungumzieni.”
Au “mpigieni muziki.”
Au “uwepo.”
Au “wazao wa.” Tnn., “mbegu ya.”
Tnn., “Neno aliloamuru.”
Tnn., “Aliuvunja kila ufito wa mikate.” Labda ni fito zilizotumiwa kuhifadhia mikate.
Tnn., “Waliitesa.”
Au “Nafsi yake iliingia katika chuma.”
Au “kama nafsi ilivyotaka.”
Tnn., “Ili awafunge.”
Aina ya mbu anayeitwa hak·kin·namʹ katika Kiebrania.
Au “miali ya moto.”
Tnn., “hofu yao.”
Au “Haleluya!” “Yah” ni ufupisho wa jina Yehova.