Zaburi 99:1-9
99 Yehova amekuwa Mfalme.+ Mataifa na yatetemeke.
Anaketi kwenye kiti cha ufalme juu ya* makerubi.+ Dunia na itikisike.
2 Yehova ni mkuu Sayuni,Naye yuko juu ya mataifa yote.+
3 Na walisifu jina lako kuu,+Kwa maana linaogopesha, nalo ni takatifu.
4 Yeye ni mfalme hodari anayependa haki.+
Umeimarisha kabisa mambo manyoofu.
Umetekeleza haki na uadilifu+ katika Yakobo.
5 Mkwezeni Yehova Mungu wetu+ na kuinama chini* mbele ya kiti cha miguu yake;+Yeye ni mtakatifu.+
6 Musa na Haruni walikuwa miongoni mwa makuhani wake,+Na Samweli alikuwa miongoni mwa wale walioliita jina lake.+
Walikuwa wakimwita Yehova,Naye alikuwa akiwajibu.+
7 Alikuwa akiongea nao kutoka katika nguzo ya wingu.+
Walishika vikumbusho vyake na amri aliyowapa.+
8 Ee Yehova Mungu wetu, uliwajibu.+
Ulikuwa Mungu uliyewasamehe,+Lakini uliwaadhibu* kwa sababu ya dhambi walizotenda.+
9 Mkwezeni Yehova Mungu wetu+Na mwiname chini* mbele ya mlima wake mtakatifu,+Kwa maana Yehova Mungu wetu ni mtakatifu.+
Maelezo ya Chini
^ Au labda, “katikati ya.”
^ Au “kuabudu.”
^ Tnn., “ulilipiza kisasi.”
^ Au “mwabudu.”