Zaburi 83:1-18
Wimbo. Muziki wa Asafu.+
83 Ee Mungu, usinyamaze;+Usikae kimya wala kutulia, Ee Mungu.
2 Kwa maana, tazama! Maadui wako wanafanya fujo;+Wale wanaokuchukia wanatenda kwa kiburi.*
3 Kwa hila wanapanga njama kwa siri dhidi ya watu wako;Wanapanga njama dhidi ya watu wako unaowathamini.*
4 Wanasema: “Njooni, acheni tuwaangamize wakiwa taifa,+Ili jina la Israeli lisikumbukwe tena kamwe.”
5 Kwa umoja wanatunga mbinu;*Wameungana* dhidi yako+—
6 Mahema ya Edomu na Waishmaeli, Moabu+ na Wahagri,+
7 Gebali na Amoni+ na Amaleki,Ufilisti+ pamoja na wakaaji wa Tiro.+
8 Pia Ashuru+ imejiunga nao;Wanawaunga mkono* wana wa Loti.+ (Sela)
9 Watendee kama ulivyoitendea Midiani,+Kama ulivyomtendea Sisera na Yabini kwenye kijito cha* Kishoni.+
10 Waliangamizwa kule En-dori;+Wakawa mbolea juu ya ardhi.
11 Wafanye viongozi wao wawe kama Orebu na Zeebu+Na wakuu* wao kama Zeba na Zalmuna,+
12 Kwa maana walisema: “Na tuimiliki nchi ambamo Mungu anakaa.”
13 Ee Mungu wangu, wafanye wawe kama mchongoma unaopeperushwa,*+Kama majani makavu yanayopeperushwa na upepo.
14 Kama moto unaoteketeza kabisa msitu,Kama mwali wa moto unaounguza milima,+
15 Wafuatie vivyo hivyo kwa tufani yako+Na kuwaogopesha kwa dhoruba yako ya upepo.+
16 Funika nyuso zao kwa aibu,*Ili walitafute jina lako, Ee Yehova.
17 Na waaibishwe na kuogopeshwa milele;Na wafedheheshwe na kuangamia;
18 Na watu wajue kwamba wewe, ambaye jina lako ni Yehova,+Wewe peke yako ndiye Uliye Juu Zaidi, juu ya dunia yote.+
Maelezo ya Chini
^ Au “wanainua vichwa vyao.”
^ Tnn., “waliofichwa.”
^ Tnn., “Wanashauriana kwa moyo mmoja.”
^ Au “Wamefanya agano.”
^ Tnn., “Wamekuwa mkono kwa.”
^ Au “korongo la.”
^ Au “viongozi.”
^ Au “kama mbaruti.”
^ Tnn., “Jaza nyuso zao aibu.”