Zaburi 109:1-31

  • Sala ya mtu anayeteseka

    • “Mtu mwingine na achukue cheo chake” (8)

    • Mungu husimama mkono wa kulia wa maskini (31)

Kwa kiongozi. Muziki wa Daudi. 109  Ee Mungu ninayekusifu,+ usinyamaze.   Kwa maana waovu na wadanganyifu hufumbua vinywa vyao dhidi yangu. Wanaongea kunihusu kwa ndimi za uwongo;+   Wananizingira kwa maneno ya chuki,Na kunishambulia bila sababu.+   Wananipinga licha ya kwamba ninawapenda;+Lakini ninaendelea kusali.   Wananilipa uovu kwa mema niliyotenda+Na chuki kwa upendo wangu.+   Mweke mtu mwovu amhukumu;Mpinzani* na asimame mkono wake wa kulia.   Anapohukumiwa, na apatikane kuwa na hatia;*Hata sala yake ihesabiwe kuwa dhambi.+   Siku zake na ziwe chache;+Mtu mwingine na achukue cheo chake cha uangalizi.+   Watoto wake* na wawe mayatima,Na mke wake awe mjane. 10  Watoto wake* na watangetange wakiombaomba,Wakitafuta chakula katika nyumba zao zilizoharibiwa. 11  Anayemdai na achukue kwa nguvu* vitu vyote alivyo navyo,Wageni na wapore mali zake. 12  Asiwepo mtu yeyote wa kumtendea kwa fadhili,*Na asiwepo mtu yeyote wa kuwahurumia watoto wake mayatima. 13  Wazao wake na waangamizwe;*+Jina lao na lifutwe katika kizazi kilekile. 14  Kosa la mababu zake na likumbukwe na Yehova,+Na dhambi ya mama yake isifutwe. 15  Yehova na akumbuke daima waliyotenda;Na afutilie mbali kumbukumbu lao kutoka duniani.+ 16  Kwa maana hakukumbuka kutenda kwa fadhili,*+Bali aliendelea kumfuatia mtu aliyekandamizwa,+ maskini, na aliyevunjika moyoIli amuue.+ 17  Alipenda kulaani, kwa hiyo laana hiyo ikampata;Hakupenda kubariki, kwa hiyo hakupata baraka yoyote. 18  Alivishwa laana kama vazi lake. Nazo zikamwagwa mwilini mwake kama maji,Mifupani mwake kama mafuta. 19  Laana zake na ziwe kama vazi analojifunika+Na kama mshipi anaovaa daima. 20  Hayo ndiyo malipo yanayotoka kwa Yehova ya mtu anayenipinga+Na ya wale wanaosema mambo maovu dhidi yangu. 21  Lakini wewe, Yehova Bwana Mwenye Enzi Kuu,Tenda kwa niaba yangu kwa ajili ya jina lako.+ Niokoe, kwa sababu upendo wako mshikamanifu ni mwema.+ 22  Kwa maana sina uwezo, nami ni maskini,+Na moyo wangu umechomwa ndani yangu.+ 23  Ninapitilia mbali kama kivuli kinachofifia;Nimekung’utwa kama nzige. 24  Magoti yangu yanalegea kwa sababu ya kufunga;Mwili wangu umekonda, unazidi kupungua.* 25  Nimekuwa kitu cha kudhihakiwa nao.+ Wanaponiona, wanatikisa vichwa vyao.+ 26  Nisaidie, Ee Yehova Mungu wangu;Niokoe kwa upendo wako mshikamanifu. 27  Na wajue kwamba mkono wako ndio uliotenda hili;Kwamba wewe, Ee Yehova, umetenda hili. 28  Waache watangaze laana, lakini wewe toa baraka. Na waaibishwe wanapoinuka dhidi yangu,Lakini acha mtumishi wako ashangilie. 29  Wale wanaonipinga na wavishwe aibu;Na wafunikwe na aibu yao kama joho.*+ 30  Kinywa changu kitamsifu Yehova kwa bidii;Nitamsifu yeye mbele ya watu wengi.+ 31  Kwa maana atasimama mkono wa kulia wa maskiniIli amwokoe kutoka kwa wale wanaomhukumu.

Maelezo ya Chini

Au “Mshtaki.”
Au “mwovu.”
Tnn., “Wanawe.”
Au “Wanawe.”
Au “Wala riba na waviwekee mitego.”
Au “upendo mshikamanifu.”
Au “Kizazi chake kijacho na kiangamizwe.”
Au “upendo mshikamanifu.”
Tnn., “Mwili wangu umekuwa mwembamba, hauna mafuta.”
Au “joho lisilo na mikono.”