Zaburi 31:1-24

  • Kumkimbilia Yehova

    • “Naiweka roho yangu mkononi mwako” (5)

    • “Yehova, Mungu wa ukweli” (5)

    • Wema mwingi wa Mungu (19)

Kwa kiongozi. Muziki wa Daudi. 31  Nimekukimbilia wewe, Ee Yehova.+ Acha nisiaibishwe kamwe.+ Niokoe kwa sababu ya uadilifu wako.+   Nitegee sikio lako.* Njoo haraka uniokoe.+ Uwe kwangu mlima ambao ni ngome,Ngome ya kuniokoa.+   Kwa maana wewe ni jabali langu na ngome yangu;+Kwa ajili ya jina lako,+ utaniongoza na kunielekeza.+   Utanitoa katika wavu walionitegea kwa siri,+Kwa maana wewe ni ngome yangu.+   Naiweka roho yangu mikononi mwako.+ Umenikomboa, Ee Yehova, Mungu wa ukweli.*+   Ninawachukia wale wanaoabudu sanamu zisizo na faida, za ubatili,Lakini mimi, ninamtumaini Yehova.   Nitashangilia sana kwa sababu ya upendo wako mshikamanifu,Kwa maana umeona dhiki yangu;+Unajua mateso makali yaliyo ndani yangu.*   Hujanitia mikononi mwa adui,Lakini unanifanya nisimame mahali salama.*   Nionyeshe kibali, Ee Yehova, kwa maana niko katika dhiki. Maumivu makali yamefanya macho yangu yadhoofike,+ na pia mwili wangu wote.*+ 10  Maisha yangu yamejaa huzuni+Na miaka yangu kilio cha maumivu makali.+ Nguvu zangu zinapungua kwa sababu ya dhambi yangu;Mifupa yangu inadhoofika.+ 11  Ninadhihakiwa na maadui wangu wote,+Hasa majirani wangu. Na rafiki zangu wananiogopa;Wanaponiona hadharani, wananikimbia.+ 12  Wameniondoa moyoni* mwao na kunisahau, kana kwamba nimekufa;Mimi ni kama gudulia lililovunjika. 13  Nimesikia uvumi mwingi wa uovu;Nimezungukwa na hofu.+ Wanapokusanyika pamoja kama kitu kimoja dhidi yangu,Wanapanga njama ya kuniua.*+ 14  Lakini ninakutumaini wewe, Ee Yehova.+ Ninatangaza: “Wewe ni Mungu wangu.”+ 15  Siku* zangu zimo mkononi mwako. Niokoe kutoka mikononi mwa maadui wangu na kutoka kwa wale wanaonitesa.+ 16  Ifanye nuru ya uso wako imwangazie mtumishi wako.+ Niokoe kwa upendo wako mshikamanifu. 17  Ee Yehova, naomba nisiaibishwe ninapokulilia wewe.+ Waovu na waaibishwe;+Na wanyamazishwe Kaburini.*+ 18  Midomo inayosema uwongo na iwe bubu,+Midomo inayoongea kwa kiburi dhidi ya mwadilifu, kwa majivuno na dharau. 19  Jinsi wema wako ulivyo mwingi sana!+ Umewahifadhia wale wanaokuogopa,+Nawe umeuonyesha mbele ya wanadamu wote, kwa niaba ya wale wanaokukimbilia wewe.+ 20  Utawaficha mahali pa siri mbele zako*+Mbali na njama za wanadamu;Utawaficha katika banda lakoDhidi ya mashambulizi ya watu wenye nia mbaya.*+ 21  Yehova na asifiwe,Kwa maana kwa njia yenye kustaajabisha, amenionyesha upendo wake mshikamanifu+ katika jiji lililozingirwa.+ 22  Lakini mimi nilishikwa na wasiwasi nikasema: “Nitaangamia kutoka mbele zako.”+ Lakini ulisikia sihi zangu za kuomba msaada nilipokulilia kwa sauti.+ 23  Mpendeni Yehova, enyi nyote mlio washikamanifu kwake!+ Yehova huwalinda waaminifu,+Lakini humlipa vilivyo yeyote anayeonyesha kiburi.+ 24  Iweni jasiri, na muwe na moyo mkuu,+Ninyi nyote mnaomngojea Yehova.+

Maelezo ya Chini

Au “Inama chini na unisikilize.”
Au “Mungu mwaminifu.”
Au “mateso ya nafsi yangu.”
Au “penye nafasi kubwa.”
Au “nafsi yangu na tumbo langu.”
Au “akilini.”
Au “kuiondoa nafsi yangu.”
Tnn., “Nyakati.”
Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.
Au “katika uwepo wako.”
Tnn., “Kutoka kwa ugomvi wa ndimi.”