Zaburi 14:1-7

  • Ufafanuzi kumhusu mpumbavu

    • “Hakuna Yehova” (1)

    • “Hakuna yeyote anayetenda mema” (3)

Kwa kiongozi. Wa Daudi. 14  Mpumbavu* husema moyoni mwake: “Hakuna Yehova.”+ Matendo yao yamepotoka, na shughuli zao zinachukiza;Hakuna yeyote anayetenda mema.+   Lakini Yehova anawatazama wanadamu kutoka mbinguniIli aone ikiwa kuna yeyote aliye na ufahamu, ikiwa kuna yeyote anayemtafuta Yehova.+   Wote wamegeuka kando;+Wote wamepotoka. Hakuna yeyote anayetenda mema,Hakuna hata mmoja.   Je, hakuna mtenda maovu yeyote anayeelewa? Wanawala watu wangu kana kwamba wanakula mkate. Hawamwiti Yehova.   Lakini watajawa na hofu kubwa,+Kwa maana Yehova yuko pamoja na kizazi cha waadilifu.   Ninyi waovu hujaribu kuharibu mipango ya mtu wa hali ya chini,Lakini Yehova ni kimbilio lake.+   Laiti wokovu wa Israeli ungetoka Sayuni!+ Yehova anapowakusanya tena watu wake waliotekwa,Yakobo na ashangilie, Israeli na afurahi.

Maelezo ya Chini

Au “Asiyetumia akili.”